Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday 19 March 2016

YANGA VS APR NI VITA LIGI YA MABINGWA


Na Mwandishi Wetu

YANGA inajitupa uwanjani leo hii kukabiliana na mabingwa wa Rwanda, APR, katika mechi ya marudiano ya raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa ambayo inaonekana kama ni vita.
Mechi hiyo itakayopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ina mvuto wa aina yake kutokana na rekodi baina ya timu ikichangiwa pia na matokeo yaliyopita.
Katika mechi yao ya kwanza jijini Kigali, Yanga ilishinda mabao 2-1 Jumamosi iliyopita, matokeo ambayo yamewaweka katika nafasi nzuri zaidi kwa kuwa sasa inahitaji sare tu ili isonge mbele.
Blogu ya brotherdanny.com inafahamu kwamba, endapo Yanga itavuka hatua ya sasa, itakutana na Al Ahly ya Misri ambayo nayo inapigana leo Ijumaa kutaka ivuke ikihitaji ushindi dhidi ya CRD Libolo ya Angola baada ya kutoka suluhu mjini Luanda.
Lakini Azam FC, ambayo inaiwakilisha Tanzania kwenye Kombe la Shirikisho, nayo iko kwenye nafasi kubwa ya kufuzu baada ya kuichapa Bidvest Wits ya Afrika Kusini kwa mabao 3-0.
Azam itacheza Jumapili hii na ikivuka hapo itakutana na Esperance de Tunis ya Tunisia ambayo leo hii iko nyumbani kucheza na Renaissance ya Chad ikiwa na ushindi wa mabao 2-0 mkononi.
Wawakilishi wa Zanzibar, JKU hawana uhakika wa kuonyesha maajabu baada ya kufungwa mabao 4-0 jijini Kampala na SC Villa.
Uhakika wa kufanya vizuri kwa klabu za Afrika Mashariki umebaki kwa Yanga, Azam na Polisi ya Rwanda na Villa ya Uganda, ingawa APR nayo ina uwezo wa kuyageuza matokeo yake na Yanga.
Polisi Rwanda ilitoka suluhu ugenini kwa Vita Club Mokanda ya Congo na inapocheza nyumbani wikiendi hii inahitaji kuutumia vyema uwanja wa nyumbani kupata ushindi.
Mabingwa wa Burundi, Vital’O walikubali kipigo cha mabao 5-1 mjini Aba, Nigeria mbele ya Enyimba na sasa wana kazi ngumu ya kupata ushindi wa mabao 4-0 mjini Kigali.
Kwenye Kombe la Shirikisho, Atletico Olympic ya Burundi haina matumaini makubwa baada ya kufungwa nyumbani mabao 2-0 na CF Mounana ya Gabon.
Katika matokeo mengine, St. Georges ya Ethiopia inaweza kufanya maajabu ikiwa itaitoa bingwa mtetezi TP Mazembe ya Congo DR baada ya kufungana mabao 2-2 Addis Ababa.
Al-Merreikh ya Sudan ilishinda ugenini 1-0 dhidi ya Warri ya Nigeria, na inahitaji sare au ushindi nyumbani ili isonge mbele, matokeo ambayo hata Zamalek ya Misri inayahitaji baada ya 1-0 ugenini kwa Union Douala ya Cameroon.
Ferroviario Maputo ya Misri, ambayo ilipita moja kwa moja kwenye raundi ya kwanza, ina kibarua ya kushinda kwa zaidi ya bao 1-0 dhidi ya AS Vita Cub ya Congo DR baada ya kufungwa bao 1-0 mwishoni mwa wiki.
ZESCO ya Zambia inakwenda Conakry, Guinea kutafuta hata sare tu dhidi ya Horoya baada ya kushinda 4-1 nyumbani kama ilivyo kwa Wydad Casablanca ya Morocco ambayo iliikung’uta CNaPS ya Madagascar mabao 5-1.
Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini ilishinda 2-0 dhidi ya Leopard ya Congo Brazzaville na wikiendi hii inahitai kukomaa ugenini ili isonge mbele kama ilivyo kwa Stade Malien ya Mali ambayo ilipata ushindi kama huo nyumbani dhidi ya Cottonsport Garoua ya Cameroon.
Ushindani mkubwa uko katika klabu nne; Olympique Khouribga ya Morocco dhidi ya Etoile Sahel ya Tunisia; na Etoile du Congo dhidi ya Etente Sportif de Setif ya Algeria. Matokeo ya mechi zote hizo wiki iliyopita yalikuwa 1-1.
Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini ilipoteza nafasi nyumbani iliporuhusu bao 1-0 mbele ya ASEC Mimosas ya Ivory Coast, sasa inahitaji kukaza buti ugenini wikiendi hii.
Ingawa ilishinda 1-0 nyumbani, lakini Club Africain ya Tunisia inahitaji kugagamala ugenini kwa MO Bejaia ya Algeria kama ilivyo kwa Al Ahly Tripoli ya Libya iliyopata ushindi kama huo nyumbani na sasa itakuwa ugenini kukabiliana na Al-Hilal ya mjini Omdurman, Sudan.
Katika Kombe la Shirikisho kunaonekana kuwa na kazi kubwa licha ya ukweli kwamba hakuna timu zilizotoka sare mwishoni mwa wiki.
MC Oran ya Algeria ilishinda 2-0 nyumbani dhidi ya Sporting Gagnoa ya Ivory Coast kama ilivyofanya ENPPI ya Misri, ambayo hata hivyo yenyewe ilishinda ugenini kwa Africa Sports huko Abidjan.
Don Bosco ya Congo DR inahitaji ushindi wa mabao 2-0 kusonga mbele baada ya kufungwa 3-1 ugenini kwa Misr Elmaqasah ya Misri.
Al-Ittihad ya Libya ilishinda 1-0 dhidi ya Medeama ya Ghana, Nasarawa ya Nigeria ilipata ushindi kama huo dhidi ya Constantine ya Algeria, Sagrada ya Angola nayo ikapata ushindi huo huo dhidi ya LD Maputo ya Msumbiji na sasa timu hizo zinatakiwa kufanya jitihada vinginevyo vibao vinaweza kugeuka zitakaocheza ugenini mwishoni mwa wiki.
Zanaco ya Zambia ina nafasi nzuri kwa ushindi wake wa ugenini wa mabao 2-1 dhidi ya jirani zao Harare City ya Zimbabwe, lakini Kawkab Marrakech ya Morocco wao wanakwenda kifua mbele kwani walishinda 3-0 nyumbani didi ya Barrack Young Controllers II ya Libya.
St Eloi Lupopo ya Congo DR ilishinda 2-1 dhidi ya Ahli Shendi ya Sudan, Stade Gabesien ya Tunisia nayo ikaifunga Kaloum Star ya Guinea 2-1 nyumbani, matokeo ambayo yanawaweka katika hatari ikiwa wataruhusu bao 1-0 watakapocheza ugenini.


No comments:

Post a Comment