Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 16 March 2016

WAZIRI MKUU ,NAIBU WAZIRI MAMBO YA NDANI ATEMBELEA KAMBI YA RUMASI-LUKOLE

Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akisalimiana na viongozi wa dini wakati alipowasili katika kambi ya Rumasi-Lukole iliyopo wilayani Ngara,mkoani  Kagera,kambi hiyo hutumika kupokea wakimbizi wanaotoka nchini Burundi ambapo baadae hupelekwa katika makambi ya Nyarugusu yaliyopo mkoani Kigoma.Waziri Mkuu yupo mkoani Kagera kwa ziara ya kikazi.

Kikundi cha ngoma za kitamaduni cha Umoja, wakicheza ngoma wakati Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa alipowasili katika kambi ya Rumasi-Lukole iliyopo wilayani Ngara,mkoani Kagera, kambi hiyo hutumika kupokea wakimbizi wanaotoka nchini Burundi ambapo baadae hupelekwa katika makambi ya Nyarugusu yaliyopo mkoani Kigoma.Waziri Mkuu yupo mkoani Kagera kwa ziara ya kikazi.
Mkurugenzi wa Idara ya Huduma kwa  Wakimbizi,iliyopo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Harrison Mseke, akisoma taarifa ya kambi ya Rumasi-Lukole mbele ya Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa, wakati wa ziara ya Waziri Mkuu kambini hapo kukagua kambi hiyo na kuongea na raia wa Tanzania na wakimbizi wa Burundi wanaoishi kambini hapo.
Naibu Waziri wa Wizara ya  Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni,akizungumza na wakimbizi wanaoishi katika kambi ya Rumasi-Lukole(hawapo pichani),wakati ya ziara aliyoongozana na Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa.Kambi hiyo iliyopo wilayani Ngara,mkoani Kagera hupokea wakimbizi kutoka nchi ya Burundi kabla ya kuwapeleka kwenye makambi ya wakimbizi ya Nyarugusu,mkoani Kigoma.
Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa,akizungumza na raia wa Tanzania pamoja na wakimbizi wa  Burundi wanaoishi katika kambi ya Rumasi-Lukole(hawapo pichani), Waziri Mkuu alitembelea kambi hiyo iliyopo wilayani Ngara,mkoani Kagera  na kuwaasa wakimbizi hao kuishi kwa kufuata sheria za nchi pasipo kuvunja amani iliyopo nchini.
Raia wa Tanzania pamoja na wakimbizi kutoka nchi ya Burundi, wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa(hayupo pichani),wakati wa mkutano aliozungumza nao katika kambi ya wakimbizi ya Rumasi-Lukole,iliyopo wilayani Ngara,mkoani Kigoma.
Waziri Mkuu, Kasssim Majaliwa(wa tatu kushoto), akimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Wakimbizi,iliyopo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Harrison Mseke (wapili kulia),wakati akielekea kukagua mabweni wanayolala wakimbizi kutoka Burundi katika kambi ya Rumasi-Lukole,iliyoko wilayani Ngara,mkoani Kagera.Wa kwanza kushoto ni Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Dk.Medard Kalemani , wa pili  kushoto ni Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni na wa kwanza kulia ni mwakilishi wa Shirika la kuhudumia wakimbizi Duniani(UNHCR),Gerald Ndabimala.

Waziri Mkuu, Kasssim Majaliwa,akikagua mabweni wanayolala wakimbizi kutoka nchini Burundi katika kambi ya  Rumasi-Lukole inayotumika kupokelea wakimbizi hao.Kambi hiyo iko wilayani Ngara,mkoani Kagera.Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Wakimbizi,iliyopo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Harrison Mseke.(Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

Imeandaliwa na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi



No comments:

Post a Comment