Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday 18 March 2016

KITUO CHA MKUBWA FELLA CHAPIGWA TAFU NA ZANTEL



Mtendaji Mkuu wa kampuni inayotoa huduma za simu Benoit Janin wa pili kutoka kushoto akiongea na wanahabari hawapo pichani katika hafla ya kuwakabidhi msaada wa komputa tatu kituo cha Mkubwa Fella. Wa pili kutoka kulia ni Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa Wizara ya Habari. Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Leah Kihimbi Hafla hiyo imefanyika jijini Dar es Salaam leo.

Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa Wizara ya Habari. Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Leah Kihimbi wa pili kutoa kushoto akikabidhi msaada wa Komputa tatu kwa wawakilishi wa Mkubwa Fella wa kwanza kulia ni Bw. Yusuph Chambuso.
Baadhi ya wasanii wa kikundi cha Yamoto Bendi wakionyesha umahiri wao wa kuimba mbele ya wanahabari wakati wa hafla ya kukabidhiwa msaada wa kompyuta tatu kwa kikundi cha Mkubwa Fella iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. (Picha zote na Benjamin Sawe).


  

Benjamin Sawe.
WHUSM.
Wananchi wametakiwa kuupenda, kuuthamini na kuuendeleza utamaduni kwa kutumia Sanaa kwani utamaduni ni mali ya jamii.
Hayo yamesemwa leo (jana) na Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Sanaa Wizara ya Habari. Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Leah Kihimbi katika hafla ya kukabidhi msaada wa Komputa tatu zilizotolewa na kampuni ya huduma za simu ya Zantel kwa mlezi wa Kikundi cha Fella na Wanawe iliyofanyika jijjini Dar es Salaam.
Akizungumza katika hafla hiyo Bi. Kihimbi alisema kazi inayofanywa na kituo cha Mkubwa Fella ni utekelezaji wa Sera ya Taifa ya utamaduni inayosisitiza ukuzaji wa sanaa katika kuendeleza na kuongeza maslahi ya wasanii.
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Zantel Mkuu wa Zantel Bw. Benoit Janin alisema sanaa ni ajira kama zilivyo ajira nyingine hivyo anaamini msaada huo utawawezesha vijana wengi kuboresha na kusambaza zaidi kazi zao za sanaa hivyo kuweza kujikimu kimaisha na kutoa ajira kwa wengine.
Akizungumza kwa niaba ya mwanzilishi wa kituo cha Mkubwa Fella Bw. Yusuph Chambuso alisema Mkubwa na Wanawe imejikita kujenga na kuhakikisha vijana wanatimiza ndoto yao na kuwasaidia wasishawishike au kujishughulisha na shughuli haramu ambazo zinapotosha maadili kwenye jamii.
Kituo cha Mkubwa na Wanawe ni kituo cha kukuza sanaa, kilichoanzishwa mwaka 2011 katika Wilaya Temeke kwa lengo la kufanya maonyesho ya sanaa na kutoa fursa kwa vijana wanaoishi kwenye mazingira magumu kuweza kukuza na kuviendeleza vipaji vyao.
Tangu kuanzishwa kwake, Mkubwa na Wanawe imefanikiwa kuibua wasanii mbalimbali kama vile Wanaume TMK na bendi ya Yamoto ambapo mpaka sasa kituo hicho kinaidadi ya vijana 102 ambao wana vipajji mbalimbali kama vile kuigiza, kuimba na kucheza ngoma.

No comments:

Post a Comment