Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday 31 January 2014

VIJANA WATAKAOIGA TAMADUNI ZA NJE KUCHAPWA VIBOKO 60 HADHARANI


Na Mwandishi Wetu, Meru

UONGOZI wa Kimila ujulikanao kama 'Rika la Kilovio' kutoka katika kabila la Wameru umepitisha sheria kali ya kudhibiti maadili kwa vijana wa kike na wa kiume, hasa wale wanaoiga tamaduni za mataifa ya nje, ambapo watakaokiuka watachapwa viboko 60 hadharani.
Hatua hiyo imekuja baada ya baadhi ya vijana katika eneo hilo la Meru kuanza tabia ya kuiga tamaduni na madili ya mataifa ya nje hali inayochangia kwa kiwango kikubwa kuporomoka kwa maadili.
Hayo yameelezwa na Akundaely Mbisse ambaye ni kiongozi wa marika ya vijana katika kabila hilo wajulikao kama "Kilovio" wakati wakimsimika na kumuingiza rasmi kiongozi wa vijana katika eneo hilo la Mareu, Herieli Mafie, mapema jana.
Mbisse alisema utaratibu huo wa adhabu ya viboko 60 utaweza kurudisha maana halisi ya kijana wa kabila hilo ambapo kwa sasa jamii ya Mkoa wa Arusha bado inaonekana kuendelea kuelemewa na tatizo la vijana wengi kuiga tamaduni za nje ya nchi huku hali hiyo nayo ikichangia hata ubaribifu wa amani ya kaya, hadi mkoa.
Alifafanua kuwa adhabu hiyo ya viboko 60 hadharani itaenda sanjari na vijana wote wenye tabia mbalimbali ambazo hazina tija kwenye jamii hiyo ya Meru kama vile uzinzi, ulevi wa kupindukia saa za kazi, wizi, mavazi yanaonesha maumbile, ukosefu wa adabu pamoja na makosa mengine ambayo chanzo chake ni kuiga maadili yasiyokuwa na tija kwennye jamii.
"Tumejipanga kuhakikisha wilaya ya Meru inakuwa na tofauti katika suala la mila kwani tunao uwezo wa kuwaweka vijana wetu wawe katika maadili mazuri, masuala kama ya uvaaji wa nguo za ajabu utakwisha na kwa hali hiyo jamii itaweza kupungza hata ujinga unaofanywa na baadhi ya vijana wachache huku wakisingizia umaskini," aliongeza Mbisse.
Mgeni rasmi katika sherehe hizo ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Arusha, John Palangyo, alisema kuna umuhimu mkubwa wa maadili ya kila kabila kurudiwa ili kuweza kuwajengea vijana uwezo wa kufanikiwa zaidi kwenye maisha yao ya kila siku.
Palangyo alisema suala la kulinda maadili lina manufaa siyo kwa vijana bali hata kwa taifa kwani kwa sasa wapo baadhi ya vijana ambao wanaharibu na kuvunja amani ya nchi kwa kuwa hawana maadili ambayo yanaanzia ngazi za marika hadi taifa.
"Hili jambo la kuwaweka vijana katika mazingira mazuri ya kimaadili linawezekana kabisa na sisi Watanzania tunatakiwa kuondokana na dhana potofu kuwa eti vijana wa sasa hawana maadili.
"Wa kuwafundisha maadili ni sisi wazee wa ukoo, rika, na hata wanasiasa, hivyo basi kila mtu anatakiwa kuzingatia hili lakini pia kuona kuwa kijana wa mwenzake ni wa kwake na kama ataharibikiwa basi atachangia uharibifu bila kujali anaharibu kwa nani," aliongeza Palangyo.

No comments:

Post a Comment