Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday 14 January 2014

Mkuu wa upelelezi Wilaya ya Newala auawa

WATU watatu akiwemo Mkuu wa Upelelezi  wa Wilaya ya Newala, ASP-Nurdini Kassim Seif (38) wamefariki dunia kufuatia ghasia zilizojitokeza jana (12.1.2014)  katika Kijiji cha Kiduni Kata ya Mtonya Tarafa na Wilaya ya Newala, Mkoani Mtwara. 
Hayo yamebainishwa leo na Issa Mnilota (ACP) ofisini kwake kwa niaba ya Kamanda wa polisi Mkoa wa Mtwara Zelothe Stephen wakati alipokuwa akiwasilisha taarifa kuhusiana na tukio hilo kuwa, tukio limetokea mnamo majira ya saa 16:45.
Aidha, amewataja marehemu hao kuwa mwananchi mmoja aliyetambulika kwa jina la Hamza Msangaluwa ambaye amefariki baada ya kupigwa risasi ya kichwa, Mkuu wa upelelezi ASP-Nurdini Kassim Seif (38) na F.8106 DC Rogert ambapo 

wote walikufa papo hapo baada ya kushambuliwa sehemu mbalimbali ikiwemo kifuani, tumboni, mapajani na miguuni  kufuatia vurugu hizo.
Aidha waliyoshmbuliwa ni F.5339 (33) na PC Issaya (34) ambapo PC Issaya amejeruhiwa vibaya sehemu ya paja ambapo kwa sasa yuko katika Hospitali ya Wilaya ya Newala kwa matibabu zaidi.
Vurugu hizo zimetokea nje kidogo ya Mjini wa Newala umbali wa km 5 barabara ya Newala – Mtwara ambapo jambazi mmoja akiwa na silaha inayosadikiwa  kuwa SMG alikwenda kituo cha mafuta cha Camel akiwa amebeba galoni na kununua mafuta ya Tshs. 2500/= na kuweka kwenye galoni alokuwa amebeba.
Mara baada ya kupatiwa mafuta hayo aliingia ndani ya jingo la kituo hicho na kuwataka wahudumu wampatie mauzo ya siku mbili yaliyofanywa kituoni hapo ambapo wahudumu walimjibu kuwa hawana fedha, fedha zote zimechukuliwa ndipo alipotoa silaha aliyokuwa ameficha ndani ya koti alilokuwa amevaa na kuwalazimisha watoe fedha.
“Kufuatia hatua hiyo jambazi huyo alianza kupekuwa na kuona fedha zilizokuwa uvunguni mwa meza ya kituo hicho na hatimaye alifanikiwa na kuweka fedha hizo ndani ya mfuko wa koti alilokuwa amevaa na kikumbilia vichakani”.Alisema Mnilota.
Hata hivyo wahudumu hao walianza kupiga kelele na kuomba msaada kutoka kwa wananchi ndipo wananchi walianza kujitokeza na kuanza kumkimbiza na wakiendelea kumfatilia kwa nyuma, jambani huyo alianza kuwafyatulia risasai lakini wananchi waliendelea kumkimbiza kiasi cha umbali wa km 8 na kuingia kwenye kichaka.
Alisema kuwa, polisi nao kwa muda huo walikuwa tayari wamepata raarifa na kuelekea na eneo la tukio ambapo jambazi huyo akiwa amejificha kwenye kichaka alifanikiwa ndipo akafanikiwa kumpiga risasi mwananchi huyo mmoja ambaye ni marehemu baada ya kubaini alipokuwa amejificha jambazi huyo hata hivyo jirani akiwepo Mkuu huyo wa upelelezi.
Aidha, jambazi huyo amefanikiwa kutoweka gizani na kuacha helment, koti, raba moja na mzula aliokuwa amevaa na mwili wa marehemu Hamza Msangalukwa  tayari umechukuliwa na ndugu zake kwa mazishi na miili mingine bado imehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya hiyo kwa taratibu zingine.
Alisema kuwa, jeshi la polisi linatoa shukrani kwa wananchi wa Kijiji na Vijiji vya jirani na watendaji wote wa Halmashauri hiyo kwa ushirikiano walioutoa na wanaoendelea kuutoa kwa jeshi la polisi.
Aidha, jambazi huyo amefanikiwa kuondoka na kiasi cha fedha Tshs. 3,299,180/= ya mauzo toka katika kituo cha mafuta cha Camel na masako mkali wa kumsaka jambazi huyo unafanyika na watatoa taarifa zingine zitakazo patikana.

No comments:

Post a Comment