Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday 21 January 2014

EZEKIEL MAIGE AJITETEA KUHUSU KUMILIKI JUMBA LA KIFAHARI

Ezekiel Maige
Nyumba yenyewe hii hapa


Wapendwa,

Salaam za pilika za maisha?

Nimeona ni vema nikawafafanulia, kwa baadhi ambao hamkufuatilia kipindi cha Medani za Siasa kilichorushwa na Star TV jana mchana.


Nimeona nifanye hivyo baada ya upotoshaji wa kitoto, uliojaa roho mbaya na chuki za makusudi uliofanywa na mtu anayejiita Kiroba kwenye mtandao wa Jamii forums.

Star TV hufaya kipindi cha Medani za Siasa kwa wanasiasa mbalimbali kila wakati. Katika vipindi vyao, huongea na mwanasiasa wanayemchagua kwa wakati huo na humuuliza mambo mengi yanayomuhusu na mambo yake ya siasa.

Ndivyo ilivyotokea kwangu weekend iliyopita.

Katika kipindi hicho, niliongea mengi kwa kujibu maswali ya mtangazaji.

Swali mojawapo aliloniuliza ni UFAFANUZI WANGU KUHUSU TUHUMA KUWA NINAMILIKI NYUMBA YA KIFAHARI.

Jamani watanzania wenzangu, nashauri sana katika masuala kama haya tuwe na utaratibu ufuatao:-
1. Kama hujaelewa au kumsikia aliyesema, basi uliza kuliko kuanza kupotosha makusudi
2. Tujitahidi kuweka pembeni siasa, hasa linapokuja suala kama hili ambalo ukweli unapatikana kwa mhusika.

Kwa kuzingatia hayo, nilichosema Star TV ni kuwa nina mkopo wa nyumba, ambayo iko hapa Dar. Bado sijaanza kuimiliki nyumba husika kwani hati bado sijakabidhiwa kwani mkopo bado sijamaliza kulipa benki. Kwa sasa, ownership ya nyumba ni ya benki.

Nimeeleza ilivyofanyika transaction husika, kuwa nilikopa 290m ndizo nilizolipa.

Wapo wanaouliza nilitoa wapi,jibu rahisi tu, ni mkopo wa kibunge ambao kila mbunge anakopa.

Wapo wanaonidhalilisha kwa kusema kuwa nimekuwa Waziri Miaka miwili na kuteneneza fedha, wananionea. Nimekuwa mbunge kwavipindi viwili, na kabla ya kuwa mbunge nilikuwa na kazi na maisha mazuri tu. Niligombea ubunge mwaka 2005 nikiwa namiliki nyumba tayari, gari 2 na mshahara mnono kwa wakati huo ulikuwa unazidi Tshs 1.5m, na cheo changu nilikuwa Mkurugenzi wa fedha na Rasilimali watu.

Sikutoka chuo na begi la vyeti kwenda kugombea ubunge. I had my life already.

Jingine kubwa tunapojadili mambo ya watu tujitahidi kukumbuka na kujiridhisha kuhusu LIABILITIES pia. Balance sheet ya mtu ina pande mbili, assets na liabilities, siyo assets tu.

Kwa taarifa yenu, nina madeni ya kufa mtu.

Nadhani mmenielewa.

Maige


HABARI ILIKUWA HIVI...

 WAZIRI AKIRI KUNUNUA NYUMBA YA MAMILIONI-"NI EZEKIEL MAIGE, ADAI ALIINUNUA KWA DOLA 410,00, LEMBELI APINGA, ASEMA ALIINUNUA KWA DOLA 700,000 TASLIMU"


Fidelis Butahe na Daniel Mjema
SIKU chache baada ya gazeti hili kuripoti taarifa za uchunguzi kwamba kuna mawaziri wawili ambao wamenunua nyumba mbili zenye thamani ya Sh1.8 bilioni, mmoja wa mawaziri hao, Ezekiel Maige wa Maliasili na Utalii ameibuka na kukiri.Maige aliliambia gazeti hili jana kuwa nyumba yake hiyo iliyoko Mbezi Beach, Dar es Salaam, ameinunua kwa Dola za Marekani 410,000 (takriban Sh656 milioni) ambazo anadai kuwa ni mkopo kutoka Benki ya CRDB.
Hata hivyo, wakati Waziri Maige akieleza kuwa nyumba hiyo ina thamani hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, James Lembeli amedai kuwa taarifa alizonazo ni kwamba ilinunuliwa kwa fedha taslimu Dola 700,000 za Marekani (takriban Sh1.1 bilioni).

Awali, habari zilizolifikia gazeti hili zilieleza kuwa Waziri Maige alinunua nyumba hiyo kutoka kwa Kampuni ya Savana Real Estate.

Mmoja wa madalali wanaouza nyumba za kampuni hiyo aliyejitambulisha kwa jina moja la Athuman (Ustadhi) alilithibitishia gazeti hili kwamba Waziri Maige amenunua nyumba moja kati ya nne zilizoko sokoni.

Hata hivyo, dalali huyo hakutaka kueleza alinunua nyumba hiyo lini na kwa gharama gani baada ya kueleza kuwa yeye si msemaji wa kampuni hiyo.

“Nyumba zipo nne na mbili zimeshauzwa. Maige kanunua nyumba moja. Nyumba nyingine mbili bado hazijauzwa na kwa sasa tunamalizia kuziwekea milango na bustani,” alisema Athuman.

Akizungumza na gazeti hili jana, Waziri Maige alisema hakununua nyumba hiyo kwa Dola 700,000 kama inavyodaiwa, bali alinunua kwa Dola za Marekani 410,000.Mbali ya kukiri, alifafanua jinsi alivyoinunua na kuonyesha nyaraka mbalimbali huku akieleza kuwa sehemu ya fedha alizonunulia, zilikuwa za mkopo kutoka Benki ya CRDB.

Alisema mwaka 2005 alipoanza kuwa mbunge alipata mkopo na yeye na wenzake watatu, waliunda kampuni ya kusafirisha mzigo ya Splendid Logistic na kuanza kununua magari matatu na baadaye magari hayo yaliongezeka na kufikia saba.
Soma zaidi:http://www.mwananchi.co.tz 

No comments:

Post a Comment