Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday 20 February 2016

WAIMBAJI WAZIDI KUMIMINIKA TAMASHA LA PASAKA

Alex Msama

Na Mwandishi Wetu
WAIMBAJI  wa nyimbo za Injili Tanzania Sifael Mwabuka na Goodluck Gozbert wamethibitisha kushiriki Tamasha la Pasaka 2016 linalotarajia kufanyika baadhi ya mikoa ya Kanda ya ziwa.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi  ya tamasha hilo, Alex Msama  waimbaji hao ni muendelezo wa kufanikisha ibad hiyo inayotarajia kufanyika mikoa ya Geita (Machi 26), Mwanza (Machi 27) na Kahama (Machi 28).
Msama alisema wanaendelea na maandalizi ya kufanikisha tamasha hilo ambalo lina dhamira ya kukemea mauaji ya walemavu wa ngozi ‘albino’ kupitia waimbaji wa muziki wa Injili watakaopanda jukwaani siku hiyo.
Msama alitoa wito kwa wakazi wa mikoa hiyo kujitokeza kwa wingi kwa sababu sehemu ya mapato ya tamasha hilo yanalengwa kusaidia kununulia baiskeli zaidi ya 100  za walemavu ambazo zitagawiwa kwa wahusika.
Aidha Msama alitaja viingilio katika mchezo huo ni shilingi 5000 kwa wakubwa na shilingi 2000 kwa watoto.
Msama alisema hivi sasa waimbaji mbalimbali waliothibitisha kushiriki tamasha hilo wanaendelea na mazoezi kwa ajili ya kujiweka sawa kabla ya tamasha hilo.

No comments:

Post a Comment