Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday 23 February 2016

HUDUMA YA MAJISAFI YAREJEA JIJINI DAR


Na Beatrice Lyimo-Maelezo
Dar es salaam
SHIRIKA LA Majisafi na Majitaka Dar es salaam (DAWASCO), imerejesha  huduma ya upatikanaji wa Maji katika maeneo yote yanayohudumiwa na mtambo wa Ruvu chini  jijini Dar es salaam, pamoja na maeneo ya mji wa Bagamoyo mkoani Pwani kutokana na mtambo huo kuzimwa kwa wastani wa saa 36 kuanzia siku ya Alhamisi 18/02/201.Akizungumzia kurejea kwa huduma hiyo, Meneja uhusiano wa DAWASCO, Bi. Everlasting Lyaro, amesema kuwa huduma ya Maji katika jiji la Dar es salaam na miji ya Bagamoyo mkoani Pwani kwa sasa yameanza kwenda kwa wananchi, na maeneo mengi ya jiji ambayo yalikosa huduma ya Maji kutokana na uzimwaji wa mtambo wa Ruvu chini.
Napenda kuwaambia wateja wetu kuwa huduma ya Maji kwa sasa imerejea kwenye maeneo mengi ya jiji baada ya matengenezo kukamilika na mtambo kuwashwa siku ya Jumapili saa 9:30 alasiri” alisema Bi. Lyaro.
Alibainisha kuwa Kuna maeneo mengine yatachelewa kupata Maji kwani mara nyingi kwa kitaalamu huwa mtambo ukizimwa kwa zaidiya saa 24 ndani ya mabomba ya kupitisha Maji hujaa hewa hivyo baadhi ya maeneo kazi ya utoaji hewa kwenye mabomba unaendelea, hivyo tuwahakikishie wananchi kuwa huduma imerejea na wataipata ndani ya muda tuliotarajia.
Awali, mtambo wa Ruvu Chini ulizimwa ili kuwaruhusu wakandarasi kutoka kampuni ya sino Hydro na mafundi kutoka DAWASCO kukarabati bomba la Maji lenye inchi 54 linalosafirisha Maji kutoka Bagamoyo mpaka matenki ya Chuo kikuu cha ardhi, Bomba lililokuwa likivuja maeneo ya Makongo Jeshini, na kusababisha maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam kukosa huduma ya Maji, Mji wa Bagamoyo vijiji vya Zinga, Kerege na Mapinga, Bunju, Boko, Tegeta, Kunduchi, Salasala, Jangwani, Mbezi Beach na Kawe.
Maeneo mengine ni pamoja na Maeneo ya Mlalakuwa, Mwenge, Mikocheni, Msasani, Sinza, Manzese, Mabibo, Kijitonyama, Kinondoni, Oysterbay, Magomeni, Upanga, Kariakoo, City centre, Ilala,, Ubungo Maziwa, Kigogo, Mburahati, Hospitali ya Rufaa Muhimbili, Buguruni, Chang’ombe na Keko

No comments:

Post a Comment