Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday, 20 September 2014

WEMBLEY KUANDAA EURO 2020

Uwanja wa Wembley



Uwanja wa Wembley ulioko Uingereza utakuwa mwenyeji wa nusu fainali ya Kombe la Euro2020, Uefa imethibitisha.
Wembley pamoja na uwanja ulioko Glasgow, Hampden Park
na ule ulioko Dublin, Aviva zitaandaa mechi 16 na tatu zingine za makundi.
Shirikisho la Soka la Uingereza lilipewa uenyeji wa mechi hiyo baada ya kuishinda shirikisho la Ujerumani.
Hata hivyo Shirikisho hilo litapata fursa ya kuandaa mechi kadha za makundi.
Haya yalibainika baada ya Uefa kutangaza viwanja 13 vitakavyoandaa mechi za Euro .
Mechi za robo fainali na tatu za makundi zitaandaliwa mjini Munich (Ujerumani), Baku (Azerbaijan), Roma (Italia) na St Petersburg (Urusi).
Miji mingine itakayoandaa mechi 3 za makundi na moja ya mkondo wa pili ni Copenhagen (Denmark), Bucharest (Romania), Amsterdam (Uholanzi), Bilbao (Uhispania), Budapest (Hungary) na Brussels (Ubeljiji).
CREDIT: BBC/MICHEZO

No comments:

Post a Comment