Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday 29 September 2014

MAMA TUNU PINDA ACHANGISHA SHS. 128.6 MILIONI KUJENGA KANISA

Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Morovian Tanzania ( KKMT)  Martin  Mwalyambwile  akimkaribisha  mke wa Waziri Mkuu Tunu Pinda wakati alipowasilia  kwenye Kanisa la Kiinjili la Usharika wa Mburahati jijini Dar es Salaam, jana kwa ajili ya kuongoza harambee ya ya kuchangia  ujenzi wa Kanisa hilo.
 Mke wa Waziri Mkuu Tunu Pinda akielekezwa kitu na  mmoja wa waumini wa Kanisa la Usharika wa Mburahati Yessaya Mwakifulefule wakati wa harambee ya kuchangia ujenzi wa Kanisa hilo iliyoendeshwa na mama Tunu Pinda jumla ya shilingi milioni 128.6 zilipatikana katika harambe hiyo iliyofanyika jana .

Mke wa Waziri Mkuu wa Mama Tunu Pinda ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye harambee ya kuchangia ujenzi wa Kanisa la Usharika wa Mburahati jijini Dar es Salaam, akiendesha harambee hiyo kwa waumini wa kanisa hilo  Kulia ni Mwenyekiti wa Kanisa Jeremia Mwakifulefule na kushoto ni familia ya Mwakifulefule.
Mke wa Waziri Mkuu mama Tunu Pinda akionyesha waumini   wa  Kanisa la Kiinjili la Ushirika wa Morovian Mburahati  Dora 1000 zenye thamani ya shilingi milioni 1.6 zilizotolewa na muumini wa kanisa hilo Tuli Mwambapa .Jumla ya shilingi milioni 128.6.zilipatikana kwenye harambee hiyo. Kulia ni Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Morovian Tanzania ( KKMT)  Martin  Mwalyambwile.

 Mke wa Waziri Mkuu Tunu Pinda (Kulia) akionyesha kiasi cha shilini milioni 2 zilizochangwa na mwenyekiti wa kanisa laKiinjilia la Usharika wa Morovian Mburahati   Jeremia Mwakifulefule (kushoto)kwa ajili ya ujenzi wa kanisa hilo.
Mke wa Waziri Mkuu mama Tunu Pinda (kulia) akimhamasisha mke wa Waziri wa Uchukuzi mama Linah Mwakyembe  wakati wa Harambee ya uchangiaji wa fedha kwa ajili ya ujenzi wa  Kanisa la Kiinjili la Morovian Mburahati  jijini Dar es Salaam, jumla ya shilingi milioni 128.6. zilipatikana kupitia Harambee hiyo iliyoendesha na Mama Pinda
Mke wa Waziri Mkuu Tunu Pinda akisikiliza ahadi ya mtoto Cecylia Mashaka (3) ambaye alichangia kiasi cha elfu 20 kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa la Usharika wa Kiinjili la Morovian Mburahati Dar es Salaam. Jumla ya shilingi milioni 128.6. zilipatikana kupitia Harambee  iliyoendesha na Mama Pinda.
Mama Tunu Pinda wa pili kutoka kulia akimsikilza kwa makini Doroth Mwakifulefule wakati alipokuwa akiahidi ahadi ya familia kwa ajili ya  mchango wa Kuchangia Ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Morovian la Mburahati jijini Dar es Salaam.Harambee hiyo ilioyoongozwa na mama Pinda zilikusanywa kiasi cha shilingi milioni 128,6.
Mke wa Waziri Mkuu  wa Jamhuri ya MuunganoTanzania Tunu Pinda akisikiliza ahadi ya moto Sharon  Yessaya aliye changia kiasi cha elf 50 kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa la Usharika wa Kiinjili la Morovian Mburahati Dar es Salaam. Jumla ya shilingi milioni 128.6. zilipatikana kupitia Harambee  iliyoendesha na Mama  Pinda.
Mke wa Waziri Mkuu Mizengo Pinda mama Tunu Pinda akisisitiza jambo kwa Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Morovian Tanzania ( KKMT)  Martin  Mwalyambwile  wakati wa Harambee ya Kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa kanisa hilo jana jumapili.  Katikati ni Katibu Mkuu Saimon Mwangasa. Jumla ya shilingi milioni 128,6 zilipatikana kutokana na harambee hiyo. 




No comments:

Post a Comment