Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday 28 September 2014

KIMBUNGA CHA SERENGETI FIESTA KUIKUMBA MBEYA LEO

Barnaba Classic kuhanikiza katika Uwanja wa Sokoine leo

Kusubiri sasa kumetosha kwa wakazi wa Mbeya na vitongoji vyake, kinywaji cha Serengeti Premium Lager kwa kushirikiana na waandaji wa tamasha la Serengeti Fiesta 2014, Primetime Promotions wameshaingia mjini humo kuporomosha burudani ya aina yake katika uwanja wa Sokoine leo.
Baada ya kugundua kwamba tamasha la Serengeti Fiesta litakuwa mkoani humo mwishoni mwa juma hili, wakazi wa mji wa Mbeya wamejipanga tayari kwa ajili ya kulipokea tamasha hilo na mashabiki wengi wameahidi kufurika katika uwanja huo.

Tamasha la Serengeti Fiesta 2014 linatarajia kuweka historia kwa kuvuta idadi kubwa ya mashabiki toka sehemu mbalimbali za mkoa huo. Kwa Mbeya tamasha hilo litatimiza shoo ya 14 kati ya 18 walizoahidi waandaaji.
Shoo hiyo inayosubiriwa kwa hamu mjini Mbeya itapomorohwa na wasanii wakali katika miondoko ya muziki wa kizazi kipya kama “Godzilla, TID, Linex, Mr. Blue, Madee, Stamina, Barnaba, Ney wa Mitego, Linah, Recho, Mo Music na Baraka Da Prince ambao wameahidi kufanya shoo ya aina ya kipekee.
“Katika kumbukumbu zetu, Mbeya ni mkoa ambao siku zote huandika historia mpya kwa kuingiza idadi kubwa ya mashabiki katika shoo za tamasha la Serengeti Fiesta. Ni matarajio yangu kuwa kwa mwaka huu pia mashabiki wetu wa mbeya watavunja tena historia ya miaka iliyopita kwa kuja kwa wingi,” alisema Rugambo Rodney, Meneja Chapa wa kinywaji cha Serengeti Premium Lager.
Akizungumza na waandishi wa habari mmoja wa wasanii ambaye anatarajiwa kutuimbuiza mjini hapa Mbeya, Godzilla alisema… “Awali ya yote, ninashukuru kuwa mmoja wa wasanii watakaotumbuiza tamasha la Serengeti Fiesta mwaka huu na zaidi ya yote, kitendo cha kutumbuiza nyumbani hakika kimenipa faraja sana. Napenda kuwahakikishia mashabiki wangu kuwa shoo yangu hapa Mbeya itakuwa moja ya shoo bora na kwamba kijana wenu wa nyumbani hatawaangusha, hivyo tukutane uwanja wa Sokoine na tuburudike kwa pamoja.”

Baada ya Mbeya, Serengeti Fiesta itaelekea Dodoma na Singida na kuhitimisha ziara yake jijini dar es Salaam hapo Oktoba 18. 

No comments:

Post a Comment