Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday 29 September 2014

UINGEREZA YAONDOA TAHADHARI KWA RAIA WAKE KUINGIA KENYA

Serikali imeondoa tahadhari iliyowekea raiya wake kuingia Kenya
Uingereza imeondoa tahadhari iliyokuwea imetoa kwa raia wake dhidi ya Kusafiri Kenya.
Tahadhari hiyo kwa ukubwa likuwa inalenga maeneo ya mitaa ya mabanda, na baadhi ya maeneo ya Pwani ambako ilihofiwa kuwa raia wa kigeni wanalengwa kwa mashambulio ya kigaidi.

Hatua hiyo ya kuondolewa tahadhari kwa raia wa Uingereza kusafiri Kenya, inaanza kutekelezwa mara moja.
Tahadhari hiyo ilikuwa imewekwa baada ya machafuko yaliyotokea nchini Kenya baada ya uchaguzi mkuu yapata miaka saba iliyopita.
Wizara ya mambo ya nje ya Uingereza imewasiliana na wizara ya ndani ya nchi hiyo kwamba hali ya hatari imeshuka kwa kiasi kikubwa.
Wizara hizo zimesema kuwa tahadhari kama hizo hutolewa kuambatana na sera za nchi hiyo za kuwatolea usalama raia wake kote duniani licha ya taifa linalozungumziwa.
Serikali ya Kenya ilikuwa imelalamika kuwa tahadhari kama hizi zinazotolewa na mataifa ya Magharibi hazina msingi na zinaathiri uchumi wa nchi hiyo.
CREDIT: BBC/SWAHILI

No comments:

Post a Comment