Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday, 12 September 2014

WAZIRI CHIKAWE ATUA KIGOMA, AKUTANA NA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA, ATEMBELEA KITUO CHA MPITO CHA WAKIMBIZI

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu, Issa Machibya (kushoto) akimkaribisha Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe katika ofisi za Mkoa huo zilizopo mjini Kigoma wakati Waziri Chikawe na maafisa wake walipofanya ziara ya kikazi katika mkoa huo. Waziri Chikawe alikutana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa huo ambapo walijadiliana masuala mbalimbali ya usalama katika wilaya zote za mkoa huo. Waziri Chikawe katika ziara yake hiyo, pia anatarajiwa kutembelea Kambi za Wakimbizi zilizopo mkoani humo. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu, Issa Machibya akizungumza  katika kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama katika Ukumbi wa Ofisi yake. Kushoto kwake ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe ambaye pia alishiriki katika kikao hicho kilichokuwa kinajadili masuala mbalimbali ya usalama mkoani Kigoma. Waziri Chikawe na maafisa wake waliwasili mkoani hum leo kwa ajili ya ziara ya kikazi. Waziri Chikawe licha ya kukutana na  Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa huo pia anatarajiwa kutembelea Kambi za Wakimbizi zilizopo mkoani humo. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama katika kikao kilichoitishwa kwa ajili yake, na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu, Issa Machibya. Katika kikao hicho kilichofayika katika Ukumbi wa Mikutano wa ofisi za Mkoa wa Kigoma, Waziri na Kamati hiyo walijadiliana masuala mbalimbali ya Ulinzi na Usalama. Waziri Chikawe na maafisa wake waliwasili mkoani humo leo kwa ajili ya ziara ya kikazi. Waziri Chikawe licha ya kukutana na  Kamati hiyo ya mkoa, pia anatarajiwa kutembelea Kambi za Wakimbizi zilizopo mkoani humo. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (watano kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Kigoma. Watatu kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu, Issa Machibya. Waziri Chikawe pamoja na kamati hiyo walifanya kikao kilichofayika katika Ukumbi wa Mikutano wa ofisi za Mkoa wa Kigoma, wakijadiliana masuala mbalimbali ya Ulinzi na Usalama ndani ya mkoa huo. Waziri Chikawe na maafisa wake waliwasili mkoani humo leo kwa ajili ya ziara ya kikazi. Waziri Chikawe licha ya kukutana na  Kamati hiyo, pia anatarajiwa kutembelea Kambi za Wakimbizi zilizopo mkoani humo. Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kulia) akiwa ndani ya moja ya nyumba za Wakimbizi waliopo katika Kituo cha Mpito cha Wakimbizi (NMC) kilichopo mjini Kigoma. Katika nyumba hiyo Waziri Chikawe alizungumza na familia ya mkimbizi kutoka nchini Kongo (kushoto) wanaoishi katika nyumba hiyo. Waziri Chikawe yupo mkoani Kigoma kwa ziara ya kikazi. Wapili kulia ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuwahudumia Wakimbizi (UNHCR), Joyce Mends-Cole. Kituo hicho kilichopo mjini humo kinawahifadhi wakimbizi zaidi ya 400 wakiwemo wanaoenda kwenye matibabu, wanaoenda nchi ya tatu, wenye matatizo ya kiusalama, na waomba hifadhi  ya muda ya ukimbizi. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kushoto) akiangalia jiko ambalo linatumika kupikia chakula cha wakimbizi katika Kituo cha Mpito cha Wakimbizi (NMC) kilichopo mjini Kigoma. Katikati ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuwahudumia Wakimbizi (UNHCR), Joyce Mends-Cole. Waziri Chikawe yupo mkoani Kigoma kwa ziara ya kikazi. Kituo hicho kilichopo mjini humo kinawahifadhi wakimbizi zaidi ya 400 wakiwemo wanaoenda kwenye matibabu, wanaoenda nchi ya tatu, wenye matatizo ya kiusalama, na waomba hifadhi  ya muda ya ukimbizi. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kulia) akimsalimia mkimbizi kutoka nchini Kongo aliopo katika Kituo cha Mpito cha Wakimbizi (NMC) kilichopo mjini Kigoma. Waziri Chikawe na maafisa wake wapo mkoani Kigoma kwa ajili ya ziara ya kikazi. Kituo hicho kilichopo mjini humo kinawahifadhi wakimbizi zaidi ya 400 wakiwemo wanaoenda kwenye matibabu, wanaoenda nchi ya tatu, wenye matatizo ya kiusalama, na waomba hifadhi  ya muda ya ukimbizi. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (wapili kulia) akiwasalimia waimba kwaya wakimbizi kutoka nchini Kongo waliopo katika Kituo cha Mpito cha Wakimbizi (NMC) kilichopo mjini Kigoma. Waimba kwaya hao walimpokea Waziri Chikawe kwa nyimbo mbalimbali wakati alipotembelea Kituo hicho cha mpito.  Kulia ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuwahudumia Wakimbizi (UNHCR), Joyce Mends-Cole. Waziri Chikawe yupo mkoani Kigoma kwa ziara ya kikazi. Kituo hicho kilichopo mjini humo kinawahifadhi wakimbizi zaidi ya 400 wakiwemo wanaoenda kwenye matibabu, wanaoenda nchi ya tatu, wenye matatizo ya kiusalama, na waomba hifadhi  ya muda ya ukimbizi. Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI

WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

No comments:

Post a Comment