Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday, 14 September 2014

UGANDA YATIBUA SHAMBULIZI LA UGAIDI



                         Vikosi vya usalama nchini Uganda
                     

 Maafisa wa polisi nchini Uganda wameimarisha usalama katika maeneo mengi ya uma katika mji mkuu wa Kampala kufuatia kukamatwa kwa washukiwa kadhaa wa makundi ya kigaidi na vilipuzi.
Msemaji wa polisi ameiambia BBC kwamba
jaribio la kutekeleza mashambulizi limetibuliwa.
Awali ,ubalozi wa Marekani mjini Kampala ulisema kuwa mamlaka ilitibua shambulizi la kigaidi lilokuwa limepangwa na washukiwa wa kundi la Alshabaab.
Ubalozi wa Marekani umewataka raia wake nchini Uganda kuendelea kukaa majumbani mwao.
Ubalozi huo tayari ulikuwa umeonya kuhusu shambulizi la kulipiza kisasi dhidi ya maeneo ya Marekani na kundi la Alshabaab ili kujibu shambulizi la angani la Marekani lililomuua kiongozi wa kundi hilo mapema mwezi huu.
BBC/SWAHILI

No comments:

Post a Comment