Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday, 14 September 2014

TASWIRA HALISI YA MKUTANO MKUU WA CHADEMA LEO MLIMANI CITY

 (Picha zote kwa hisani ya JamiiForums)


Mkutano Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo unaendelea pale Mlimani City jijini Dar es Salaam ambao utamchagua Mwenyekiti pamoja na makamu wake wa Bara na Zanzibar.

Tayari chama hicho kimefanya chaguzi mbalimbali za mabaraza yake kama Baraza la Wazee, Baraza la Vijana (Bavicha) na Baraza la Wanawake (Bawacha).
Pia jana vikao vikuu vya chama - Kamati Kuu na Baraza Kuu vimefanyika.
Mkutano wa leo umeanza rasmi tangu saa 4 asubuhi ambapo waalikwa mbalimbali wamehudhuria wakiwemo Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia, Makamu Mwenyekiti wa CCM, Phillip Mangula, Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Francis Mutungi, mabalozi mbalimbali na viongozi wa vyama rafiki wa Chadema kutoka nchi mbalimbali.

Tutaendelea kuwaletea yanayojiri...

No comments:

Post a Comment