Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Thursday, 18 September 2014

RAIS KIKWETE AWAPANDISHA VYEO MAJENERALI SABA

Rais Dk. Jakaya Kikwete

Dar es Salaam. Rais Jakaya Kikwete amewapandisha vyeo maofisa saba wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), wenye vyeo vya Brigedia Jenerali kuwa Meja Jenerali.
Taarifa iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano ya JWTZ,
ilisema Rais amewapandisha vyeo maofisa hao kuanzia Septemba 12, mwaka huu kwa mujibu wa Kanuni za Majeshi ya Ulinzi, aya ya 7.01 Kifungu cha tatu.
Taarifa hiyo ilisema Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange aliwavisha vyeo maofisa hao kwa niaba ya Rais Kikwete katika sherehe zilizofanyika jana katika Makao Makuu ya JWTZ.
Waliopandishwa vyeo ni pamoja na Gaudence Milanzi, James Mwakibolwa, Ndetaulwa Zakayo, Venance Mabeyo, Simon Mumwikuwa, Issa Nassor na Rogastian Laswai.
Taarifa hiyo ilisema Meja Jenerali Milanzi ameteuliwa kuwa Mkuu wa Chuo cha Ulinzi wa Taifa (NDC). Nafasi hiyo ilikuwa ikishikiliwa na Luteni Jenerali Charles Makalala ambaye amestaafu.
CREDIT: MWANANCHI

No comments:

Post a Comment