Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday, 13 September 2014

MWIGULU NCHEMBA ALIA NA WAAJIRI WASIOWASILISHA MICHANGO YA WAFANYAKAZI

Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba

Na Mwandishi Wetu, Brother Danny Blog
ARUSHA: NAIBU Waziri wa Fedha, Mwigulu  Nchemba ameitaka mifuko ya hifadhi ya jamii kuwachukulia hatua za kisheria ikiwemo kuwafikisha mahakamani  waajiri  ambao wamekuwa hawawasilishi michango ya wanachama wao
 hali ambayo imekuwa ikichangia kuwepo kwa migogoro ya mara kwa mara.
Aliyasema hayo wakati akifungua mkutano wa 24 wa wanachama wa hifadhi ya mfuko wa jamii wa PPF unaoendelea mjini hapa.
Alisema kuwa, hali hiyo imekuwa ikichangia umaskini mkubwa kwa kuwa wapo baadhi za wanachama ambao wanakosa haki zao za msingi kutokana na makato yao kubaki kwa waajiri kwa kipindi cha miaka mingi tofauti na sheria ya mifuko inavyosema.
Nchemba aliongeza kuwa, kitendo cha mifuko  ya jamii  kuendelea kulalamikia hali hiyo ya waajiri kutowasilisha michango hiyo, bado haitoshi ila kinachotakiwa kuanzia sasa ni kuwachukulia hatua ili kukomesha tabia hiyo ya kuwanyanyasa baadhi ya wafanyakazi.
"Kila ninapokwenda kwenye mikutano ya mifuko ya hifadhi ya jamii nimekuwa nikikutana na changamoto hiyo ambayo ni kilio cha mifuko yote nchini, sasa umefika wakati kuangalia sheria zinasemaje kwani wanaoteseka ni Watanzania wenzetu," alisema .
Alifafanua zaidi kuwa, kuanzia sasa wizara ya fedha imeweka mikakati mbalimbali ya kuhakikisha kuwa inawafuatilia baadhi ya waaajiri wanaowanyima wafanyakazi haki zao za msingi na kuhakikisha kuwa wote wanachukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kufikishwa mahakamani.
Aidha aliitaka mifuko hiyo kuwasilisha taarifa ya mapato na matumizi kila mwaka ili kuwezesha wanachama wake kuwa na imani na chombo chao  na hivyo kuepuka migogoro ambayo imekuwa ikichangiwa kutokana na kutokuwepo kwa taarifa hizo kwa wakati.
Naye Mwenyekiti  wa Bodi ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Ramadhan Kijja ,alisema kuwa, mfuko huo umeanzisha utaratibu wa kusomesha watoto wa wanachama wao toka elimu ya awali hadi kidato cha sita ikiwa ni njia mojawapo ya kuendeleza wasomi wanaonufaika na mfuko huo.
Alisema kuwa,  hadi sasa hivi wametumia kiasi cha shs 750 milioni ambazo zimewanufaisha wanafunzi elfu moja mia moja ambao wanapata elimu kuanzia ngazi ya awali hadi kidato cha sita ambapo hali hiyo imewaondolea mzigo wanachama wake hususani wale  waliokuwa hawana uwezo.
Alifafanua kuwa,mbali na kuwasaidia wanafunzi hao  pia thamani ya mfuko wa PPF  umeongezeka kutoka trilioni 1.09  kwa mwaka 2012 hadi kufikia trilioni 1.48 kwa mwaka 2013 sawa na ongezeko la asilimia 36.27.


No comments:

Post a Comment