Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday, 15 September 2014

AZAM ITAMUOTA JAJA, KUMBE NI KIMBUNGA HATARI!



 Na Sosthenes Nyoni na Vicky Kimaro, Mwananchi
Jumatatu,Septemba15  2014 


Dar es Salaam. Mshambuliaji Genilson Santana ‘Jaja’ jana alikuwa na kazi moja ya kunyamazisha wanaombeza baada ya kufunga mabao mawili na kuiongoza Yanga kuichapa Azam 3-0 katika mchezo wa Ngao ya Jamii kwenye Uwanja Taifa, Dar es Salaam.
Mshambuliaji huyo Mbrazili alifunga mabao hayo mawili ndani ya
dakika tisa katika kipindi cha pili na Simon Msuva akafunga bao lililohitimisha ushindi huo mnono dhidi ya moja ya timu bora nchini.
Jaja, ambaye aliwasili msimu huu baada ya kocha Mbrazili Marcio Maximo kuajiriwa Yanga alifunga bao la kwanza katika  dakika 56 alipounganisha krosi ya chini ya Msuva, aliyeingia kipindi cha pili.
Mshambuliaji huyo wa kati aliongeza bao la pili katika dakika ya 65. Alikuwa amepewa pasi upande wa kulia wa eneo la penati. Aliufuata, akamwangilia kipa Mwadini Ali na baadaye kupiga kiki kwa kuubetulia mpira juu ya kipa huyo ambaye alikuwa ametoka kwenye mstari wake akiwa amebana upande wa kushoto.
Mashabiki na wachambuzi wengi wa soka wamekuwa wakimbeza Jaja kuwa ni mchezaji mzito, lakini mabao ya jana yatawafanya wafikirie upya uwezo wake.
Msuva alihitimisha karamu hiyo ya mabao katika dakika ya 87. Alikuwa ametanguliziwa mpira mrefu na Hussein Javu, lakini Mwadini alitoka vibaya golini na kurusha daruga kwa lengo la kuubutulia mbele mpira na alipoukosa, Msuva aliufuata na ‘kuuburuzia’ mpira golini wakati kipa huyo akigaagaa chini.
“Wachezaji walicheza vizurina wamepata matokeo mazuri. sasa naanza maandalizi kwa ajili ya mechi ya Mtibwa Sugar inayofundishwa na kijana wangu,” alisema Maximo baada ya mchezo.
Azam ilichezesha mshambuliaji mmoja, Didier Kavumbangu wakati Kipre Tchetche na Leonel  waliongeza nguvu katika safu ya kiungo iliyokuwa na wachezaji watano, lakini ikamudu kutengeneza nafasi ambazo hazikutumiwa vizuri.
“Ni vizuri kwamba tumepata matokeo haya mapema kwa sababu yatatusaidia kujirekebisha kabla ya kuanza ligi,” alisema kocha Mcamerooni wa Azam, Joseph Omog.
Kavumbagu, Tchetche na Leonel kupata nafasi nyingi za kupiga mashuti, lakini yaliishia mikononi mwa Dida.
Yanga ilipeleka mashambulizi mengi kupitia upande wa kulia ambako Mrisho Ngasa na Haruna Niyonzima walikuwa wakipita kirahisi na kutuma krosi ambazo hata hivyo hazikuunganishwa wavuni.
Mwamuzi Mbelwa alitoa kadi za njano kwa nahodha wa Azam, Abubakari Salum na mwenzake wa Yanga, Nadir Haroub ‘Canavarro’ kwa mchezo mbaya.
Kwa mara ya kwanza baada ya filimbi ya mapumziko winga wa Yanga, Ngasa alibadilishana jezi na Abubakari ‘Sure Boy’.
Azam FC:  Mwadini, Shomari Kapombe, Erasto Nyoni/Gadiel Michael, David Mwantika, Aggrey Moris, Bolou Michael, Himid Mao/Khamis Mcha, Salum Abubakar ‘Sure Boy’, Kavumbagu, Tchetche/Ismail Diara na Leonel Saint Preux/Kelvin Friday.

Yanga: Dida, Said Juma/Hassan Dilunga, Oscar Joshua, Canavaro, Kelvin Yondani, Mbuyu Twite, Said Juma, Niyonzima/Hamis Kiiza, Jaja/Javu, Ngassa/Omega Seme na Nizar Khalfan/Msuva.

CREDIT: MWANANCHI: KIMBUNGA JAJA CHAIKUMBA AZAM

No comments:

Post a Comment