Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday, 16 September 2014

SERIKALI YAJIPANGA KUFUTA ASASI ZA KIJAMII



Dar es Salaam. Wizara ya Mambo ya Ndani imetishia kuvifutia usajili vyama vyote vya kijamii vinavyokiuka kanuni na sheria kuanzia Oktoba mwaka huu.
Msemaji wa wizara hiyo, Isaac Nantanga alisema jana kuwa kumekuwa na uvunjaji wa Sheria Namba 337
inayosimamia vyama hivyo na kwamba Serikali imeamua kuviondoa vile vyote visivyo na sifa za kuendelea kuwapo.
“Sababu zitakazofanya chama kifutwe kutoka katika daftari la msajili wa vyama vya kijamii ni kufanya shughuli tofauti na zile zilizoandikishwa katika katiba ya chama husika,” alisema Nantanga.
“Pamoja na hiyo, hata vile visivyowasilisha taarifa za utendaji kazi, mapato na matumizi ya fedha zake sambamba na kutolipa ada za mwaka kwa wakati, navyo vitakuwa katika mkumbo huo.
“Wizara itachapisha majina ya vyama vyote vya kijamii vilivyo katika daftari la kudumu la msajili ili kutoa nafasi ya miezi mitatu kwa vyama hivyo kujitathmini kabla utekelezaji haujafanywa.”
Daftari hilo kwa sasa lina vyama 9,554 vya kijamii nchini vinavyojumuisha vyama 956 vya kidini na vingine 8,598. Taarifa hiyo inasema kuwa kila chama kinatakiwa kuhakikisha kuwa kinatekeleza matakwa yote ya kisheria yanayokiongoza kama inavyotakiwa.
“Zoezi hili litawezesha uanzishwaji wa mfumo wa kisasa wa taarifa za pamoja (database) utakaoboresha mawasiliano kati ya msajili na vyama husika. Pia itajumuisha uhakiki wa vyama hivyo na kuviondoa visivyostahili,” alisema.
Baadhi ya vyama hivyo vimedaiwa kubadili katiba zao pasipo kuridhiwa na msajili, jambo linalochangia kutotambuliwa kwa shughuli zake mpya zilizoainishwa na katiba hizo.
CREDIT: MWANANCHI

No comments:

Post a Comment