Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 14 September 2016

GHARAMA ZA CHAKULA, MALAZI VYUO VIKUU NI SHS. 8,500 KWA SIKU

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhandisi Stella Manyanya

Na BEATRICE LYIMO, MAELEZO, DODOMA
Serikali imekuwa ikifanya utafiti juu ya gharama halisi na maisha ya wanafunzi wa vyuo vikuu ambazo hujumuisha gharama za chakula na malazi vyuoni.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhandisi Stella Manyanya alipokuwa akijibu swali la Mhe. Zainab Katimba (Viti Maalumu) lililohusu mpango wa Serikali kuongeza fedha kwa wanafunzi hao.Naibu Waziri Mhandisi Manyanya amesema kuwa Serikali kupitia Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu ilifanya utafiti katika vyuo vyote nchini ili kujua gharama halisi za chakula na malazi ambapo utafiti huo umebainisha kuwa gharama hizo ni kati ya 8,000 na 8,500 kwa siku.
Aidha, ameongeza kuwa utafiti huo hufanywa kila baada ya miaka miwili, hivyo, Wizara yake itafanya utafiti mwingine ili kubainisha gharama halisi za chakula na malazi ambapo matokeo ya utafiti huo yatatumika kupanga viwango vya fedha atakazolipwa mwanafunzi kwa kuzingatia gharama halisi pamoja na upatikanaji wa fedha.
Mbali na hayo, akijibu swali la Mhe. Zainabu Mwamwindi lililohusu mpango wa Serikali kuviwezesha vyuo vikuu nchini kufanya utafiti Mhandisi Manyanya amesema kuwa Serikali imekuwa ikitenga fedha hizo kupitia Mfuko wa Taifa wa Uendeshaji wa Sayansi na Tekinolojia (MTUSATE) unaoratibiwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH).
“Fedha za utafiti kutoka kwenye mfuko huo zimekuwa zikitumiwa na watafiti wa ndani ya nchi wakiwemo watafiti kutoka vyou vikuu ambapo utaratibu ni kwamba miradi hii ya utafiti hufadhiliwa kwa misingi ya ushindani kuoitia ubora wa maandiko ya miradi ya utafiti”, amefafanua Mhandisi Manyanya.
Mbali na hayo vyuo vikuu vyote nchini vinatakiwa kutenga fedha kupitia bajeti zao pamoja na kutafuta wafadhili na wadau wa maendeleo kwa ajili ya kuendesha shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwemo kufanya utafiti.

No comments:

Post a Comment