Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday 6 September 2015

BAKWATA YAKERWA NA LUGHA YA MATUSI


NA JOHN NGUNGE
Viongozi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), Wilaya ya Arumeru, mkoani Arusha, wamekemea wagombea wa vyama vya siasa wanaotumia lugha za kashfa katika kampeni hali inayoweza kutishia uvunjifu wa amani.
 
Mwenyekiti wa Bakwata Wilaya ya Arumeru, Ustadhi Haruna Hussein alisema, wanasiasa hao wanachopaswa kufanya ni kunadi sera na sio kutukanana kwenye majukwaa hali ambayo inaashiria kuwapo kwa uvunjifu wa amani kutokana na mienendo yao.
 
Aidha aliwataka wanasiasa hao kunadi sera zao kwa wananchi kuwa watawafanyia mambo gani pindi watakapochaguliwa badala ya kusimama kwenye majukwaa na kuanza kutoa lugha za kashfa na matusi kitendo kinachochagia wananchi kukosa imani nao.
 
Alisema viongozi hao ni kioo kwa jamii hivyo wanapaswa kuonyesha dira ya uongozi na sio kuwa na matusi na kashfa.
 
Naye mjumbe wa Bakwata Wilaya ya Arumeru, na Kaimu Sheikh wa Msikiti wa Patandi, Ally Ramadhani Haji, alisema madhara ya kutaja mambo ya aibu za watu majukwaani ni kutengeneza chuki zisizokuwa na maana, kwa sababu dunia inapita kwenye kipindi kigumu na moja ya mambo yanayosababisha chuki na vurugu ni siasa za chuki baina ya viongozi ambapo mwisho wa siku watu wanaingia kwenye matatizo.
 
Kwa upande wake, Sheikh wa Wilaya ya Arumeru, Ally Isa Ibrahimu alisema, viongozi hawatakiwi kufarakana na kutukanana pamoja na kuchafuana kwenye kampeni bali wawe wamoja katika mambo yao huku wakizungumzia suala zima la amani ya nchi ili kufanyika kwa kampeni za kistaarabu.
 
Alisema katika kuelekea kipindi hiki cha uchaguzi vyama vya siasa pamoja na viongozi wa siasa wanapaswa kutangaza amani ya nchi, kwani jamii haipo tayari kuona viongozi hao wa kisiasa wakifanya kampeni chafu zinazochangia        viasharia vya amani.
 
Sheikh wa Msikiti wa  Patandi,  Abdalah Said Omar alisema, kwa ujumla baraza hilo wilayani Arumeru halifurahishwi na  siasa chafu zinazofanywa na baadhi ya viongozi wa siasa ikiwamo kutoleana lugha za matusi hatua ambayo inaipeleka nchi pabaya hivyo ni wajibu wao kuhakikisha kuwa wanazungumza maneno mazuri yenye kuiletea nchi amani.
 
CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment