Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday, 6 December 2014

TRADE CRAFT YATOA MAFUNZO KWA WAJASIRIAMALI WAFUGAO NYUKI SIKONGE

 
Na Hastin Liumba, Sikonge

SERIKALI wilaya ya Sikonge mkoani Tabora imesema itaendelea kuboresha na kuongeza thamani ya zao la Nyuki sanjari na kuagiza kila kaya kuwa na mizinga miwili ya Nyuki ili kuweza kujiongezea kipato.

Mkuu wa wilaya ya Sikonge Hanifa Selengu alisema hayo kwenye mafunzo kwa wajasiliamali wanaushirika wanaofuga Nyuki, mafunzo ambayo yaliendeshwa na shirika lisilo la kiserikali la TRADE CRAFT toka nchini Uingereza.
Selengu alisema serikali imeweka jitihada zake kuhakikisha sekta ya Nyuki wilayani Sikonge inafanikiwa na sasa imeanzisha Mashamba darasa sanjari na kuyasimamia kwa ukaribu.
Hata hivyo aliwaomba washiriki wamafunzo hayo kutumia elimu, fursa na mafunzo watakayopata ili waondokane na umasikini wao wa kutumia sekta ya ufugaji Nyuki kupata kipato.
Mkuu huyo wa wilaya alisema hadi sasa Sikonge imezalisha asali tani 287 hadi kufikia mwaka 2014 lakini akawataka wafugaji hao kuendelea kujiunga kwenye vyama vya Ushirika.
Alisema hadi kupindi hiki zinahitajika tani 20 za asali ambazo ni sawa na Ndoo 600 za ya asali na hadi sasa jumla ya Ndoo 400 zimeshapatikana.
Kwa upande wake Afisa Mwezeshaji wa shirika la TRADE CRFT ‘Beet Project’  Job Chimwaga alisema hadi sasa katika wilaya ya Sikonge katika mafunzo hayo wamefikiwa wafugaji Nyuki 300 wakiwemo wanawake 121 na wanaume ni 179.

Alisema wilaya hiyo hadi sasa ina jumla ya wafugaji Nyuki wapatao 2,160 ambao wanatambulika na aliwataka kutumia mafunzo wapatayo kuzalisha asali bora na kuepuka uchakachuaji.

No comments:

Post a Comment