Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday, 6 December 2014

TAMASHA LA KRISMAS MBEYA, IRINGA NA SONGEA LAIVA

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Muimbaji wa nyimbo za injili nchini Edson Mwasabwite anaetamba kwa sasa na kibao chake kijulikanacho kwa jina la ‘Ni kwa neema na rehema’ amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi katika Tamasha la Krismas litakalofanyika katika mikoa ya Mbeya, Iringa na Songea Desemba mwaka huu.

Amesema tayari amejipanga kikamilifu kukonga nyoyo za mashabiki wake katika tamasha hilo linalotarajiwa kufanyika tarehe 25, 26 na 28 hivyo mashabiki zake wajitokeze kwa wingi kupata burudani ya nguvu kutoka kwake.
Ameongeza kuwa kwa mwaka huu watanzania wakae mkao wa kula kwa kusifu na kuabudu katika Tamasha la Krismas kwani tayari amezindua albamu yake ya pili ijulikanayo kwa jina la ‘Asilimia mia Mungu amenihurumia’ yenye nyimbo tisa.
‘Nimejipanga vizuri kutoa burudani kwa mashabiki zangu katika tamasha la mwaka huu la krismas kwani maandalizi ni mazuri, safari hii itakuwa zaidi ya mwaka jana kwa sasa nina nyimbo nyingi zitakazowabariki mashabiki zangu na tayari nimeshazindua albamu mpya’ alisema Mwasabwite.
Aidha amempongeza Mkurugenzi wa Makampuni ya Msama Promotions kwa kuweza kuandaa tamasha kubwa la kikristo lenye mafanikio makubwa kwa kuweza kuwakutanisha waimbaji mbalimbali kutoka ndani na nje ya Tanzania kwa lengo la kutangaza injili nchini kwetu.
Hata hivyo ameviomba vyombo vya habari kutoa sapoti ya kazi zao ili waimbaji wa nyimbo za injili waweze kuitangaza injili ulimwenguni kote na kusisitiza umoja na mshikamano kwa waimbaji wa muziki wa injili.
"Makampuni ya Msama yanaaminika na kukubalika kwa watanzania na nchi nyingine za jirani ndio maana hata tamasha linafanikiwa, tunaomba wananchi waendelee kununua kazi zetu, media mtusapoti ili tufike mbali, na kwa waimbaji wenzangu tuwe na umoja ili tufanikiwe katika kazi zetu’ alisema.
Kwa upande wa Msama Video Production wamesema kwa mwaka huu wamejipanga vizuri katika Tamasha la Krismas kwani wanavifaa vipya na vya kisasa vyenye uwezo mkubwa wa kufanya kazi katika mazingira yoyote yale na wafanyakazi wakutosha wenye ueledi katika fani hiyo.
Uongozi wa Msama Video Production unawaalika umma wa watanzania kushiriki katika Tamasha la Krismas la mwaka huu litakalofanyika nyanda za juu kusini.


No comments:

Post a Comment