Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday, 6 December 2014

TRA TABORA YAVUKA LENGO LA MAKUSANYO 2013/2014

  
Na Hastin Liumba, Tabora
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Tabora imevuka lengo la makusanyo ya mapato kwa mwaka wa fedha wa 2013/2014 na kufanikiwa kukusanya sh Bilioni 15.47 sawa na asilimia 102.

Meneja wa mamlaka ya mapato (TRA) mkoa wa Tabora Paulo Werema Laurant alisema hayo wakati akifanya mahojiano na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake mkoani hapa.
Laurant alisema katika mwaka wa fedha wa 2013/2014 mkoa uliweka lengo la kukusanya sh Bilioni 15.14 na walifanikiwa kukusanya sh Bilioni 15.47 sawa na asilimia 102.
Alisema TRA kupitia mkakati wake wa nne wa miaka mitano 2013/2014-2017/18 ambao upo katika mwaka wa pili wa utekelezaji wake una lengo la kuongeza pato la taifa kwa asilimia 19.9 kufikia mwaka 2017/2018 ikiwa ni sehemu ya azma ya kuongeza mapato ya ndani na kupunguza sehemu ya utegemezi.
Laurant alibainisa kwa mwaka wa fedha wa 2014/2015 mkoa umepewa jukumu la kukusanya   kiasi cha sh Bilioni 19.36 ikiwa ni ongezeko la asilimia 22 ya lengo la mwaka wa fedha wa 2013/2014 na hiyo ni moja ya changamoto kwa mkoa kwani kuna vyanzo vichache vya mapato.
Alitaja changamoto nyingine ni suala la elimu bado ni changamoto kwa walipa kodi hivyo kupelekea biashara nyingi kukosa kumbukumbu nzuri.
Aidha nyingine ni mwitikio mdogo kwa raia kutoa taarifa za wakwepa kodi,mwitikio mdogo katika ununuzi wa mashine za kutolea risiti (EFDs) awamu ya pili ikiwa lengo ni kusajili wafanyabiashara 3,716 kufikia mwezi Disemba 31,2013 kwani ni wafanyabiashara 69 tu sawa na asilimia 1.86 ndiyo wamenunua mashine hizi.

Hata hivyo alisema wamejipanga kukabiliana na changamoto hizo ikiwa ni kuendelea kutoa elimu,kufuatilia kwa ukaribu matumizi ya mashine na kupanua wigo wa kodi kwa kusajili biashara zote zinazostahili.

No comments:

Post a Comment