Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday, 6 December 2014

SIKONGE WATAKIWA KUJENGA VYOO BORA

Hii ni taswira ya vyoo vingi vya vijijini na hata katika miji midogo nchini

Na HastinLiumba, Sikonge

WAKAZI wa wilaya ya Sikonge mkoa wa Tabora wameagizwa kila kaya kuwana vyoo bora ili kujilinda na magonjwa yatokanayo na uchafu.

Mkuu wa wilaya ya Sikonge Hanifa Selengu alisema hayo kwenye kilelecha siku ya Mazingira duniani ambacho kilifanyika katika kata ya Molewilayani humo.
Selengu alisema hali ni mbaya katika baadhi ya kaya kwani inaonyeshawakazi hao wanajisadia vichakani kwani ni asilimia 70 ya magonjwayanatokana na uchafu na hivyo ni vyema wananchi sasa wakabadilika nakuwa na vyoo bora.
Alisema magonjwa kama Ebola,kuharisha na homa za matumbo zinatokana nauchafu hivyo ni vyema wananchi wakabadilika na kuachana na tabia zakuwa na imani potofu.
“Ni kaya 89 katika kijiji cha Usanganya hapa tunapoadhimisha siku hiii...bado ni asilimia ndogo zenye vyoo kulinganisha na wakazi wakata hiyo hii n hatari iliyo mbeleni kwetu tujenge vyoo sasa,”alisema
Selengu.
Kaimu afisa afya wa wilaya ya Sikonge Laurent Lushekya katika taarifayake alisema hadi mwaka 2013 kaya ambazo hazina vyoo  zimepunguakutoka asilimia 15.5 mwaka huo hadi asilimia 13.8.
Alisema kaya zenye vyoo bora zimeongezeka kutoka asilimia 10.5 mwaka2013 hadi asilimia 25.8 kwa mwaka 2014.
Alisema wilaya imepewa malengo ya kitaifa ya kuwa na vyoo bora 1,458ifikapo mwaka 2016 na kutakiwa kufikia asilimia 50 ambapo ni vyoo 729ifikapo Desemba mwaka 2014.
Lushekya aliongeza takwimu zilizopo zinaonyesha wilaya imefikiaasilimia 53 kuwa na vyoo bora 778 katika vijiji vilivyo katika kampeniya susafi wa mazingira.
Hata hivyo alisema wamejipanga kuhamasisha vijiji vyote vya wilaya yaSikonge kuhusiana na afya ya usafi na mazingira.


No comments:

Post a Comment