Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday, 7 September 2016

OFISI YA MAKAMU WA RAIS YAKANUSHA TAARIFA ILIYOSAMBAZWA KWENYE MITNDAO



Ofisi ya Makamu wa Rais inakanusha taarifa inayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kwamba Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan, ameomba kujiuzulu nafasi yake na kwamba taarifa hiyo ni ya uzushi na uongo haina ukweli wowote.




JAMHURI  YA  MUUNGANO  WA  TANZANIA
OFISI YA MAKAMU WA RAIS
Anuani ya Simu: “MAKAMU”                             Ofisi ya Makamu wa Rais,
Simu Na.: 2116919                               6 Barabara ya Albert Luthuli,                                                                                                   
Fax Na:    2116990                                             S.L.P.  5380,
Unapojibu taja:                                                11406 Dar es Salaam,

                                                                                                                        6 Septemba, 2016
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
YAH: KUKANUSHA TAARIFA INAYOSAMBAZWA KWENYE
MITANDAO MBALIMBALI YA KIJAMII

Ofisi ya Makamu wa Rais inakanusha taarifa inayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kwamba Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan, ameomba kujiuzulu nafasi yake na kwamba taarifa hiyo ni ya uzushi na uongo haina ukweli wowote.

Taarifa hiyo ni ya uchochezi inayolenga kuliweka Taifa kwenye taharuki.  Mhe. Makamu wa Rais yuko bega kwa bega na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kufanya kazi zao kwa mujibu wa Katiba ya nchi ili kuwaletea wananchi maendeleo.

Ofisi ya Makamu wa Rais inawataka wananchi na Watanzania kwa ujumla kupuuza taarifa hiyo ambayo inalenga kupotosha umma kuhusu ushirikiano mzuri uliopo baina ya Viongozi wetu.

Mwisho, Ofisi ya Makamu wa Rais inawasihi Watanzania kufanya kazi kwa bidii na wajiepushe na vitendo vinavyolenga kuvuruga amani na utulivu nchini.

Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais

Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment