Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday 4 September 2015

WANANCHI WATOA ARIDHI EKARI 42 ZA UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA


Na Hastin Liumba, TaboraWANANCHI  wa kata  ya Ipuli Manispaa ya Tabora waliokuwa na mgogoro wa ardhi  dhidi ya Halmashauri  ya manispaa ya Tabora katika eneo la Uledi wametoa Hekari (40) za Ardhi  yao na kuikabidhi serikali kwa ajiri ya  ujenzi  wa Hospitali ya wilaya ya Tabora Mjini.

Hatua  hiyo  imefuatia  baada  ya maridhiano  kufanyika  dhidi  ya pande  hizo mbili zilizokuwa na mgogoro  wa aridhi  uliodumu  kwa zaidi  ya miaka mitano  bila kupata  ufumbuzi  wa mgogoro  huo.
Wakizungumza kwanyakati tofauti katika zoezi la upimaji hekari  hizo walisema malumbano  hayo hayana umuhimu na kuona kutoa hekari hizo ili waweze kunufaika na huduma bora ya afya itakayo hudumia wananchi wengi zaidi.
Amani  Mbwambo  Mkazi wa Tabora  manispaa alisema kwa sasa mgogoro huo umekwisha na kuwataka wananchi kuunga mkono maridhiano  hayo iliwaweze kupata maendeleo  haraka.
Azizi  Kitamanwa mkazi wa Ipuli  uledi Tabora manispaa alisema serikali inapaswa kuwa inatatua haraka migogoro  ya aridhi ili wananchi waweze kuendelea na maendeleo  ya kijamii.
Afisa  Mipango  miji  manispaa  ya Tabora  Godard  Mwakalukwa alisema ili migogoro  ya aridhi  iweze kupungua suala  la ushirikishwaji wananchi lizingatiwe  na kupewa uzito  na viongozi  wa serikali.
Ofisa huyo aliwapongeza wananchi  hao kwa kufikia maamuzi hayo ya kukata hekari 40 na kuikabidhi serikali dhidi ya ujenzi wa hospitali ya wilaya kuwa ni jambo la kujivunia.
Kwa upande  wake  Mkurugenzi  wa  Kampuni  ya  Ardhi  Plan  Limited Gombo  Samandito  alisema  tayari  Kampuni  yake  kwa  kushirikiana na  Wananchi  wa  eneo  hilo  la  Uledi   imekwishapima  viwanja zaidi  ya  elfu  nane  kwa  ajili  ya  makazi  ya  Wananchi huku ikitenga  maeneo  ya  huduma  za  kijamii  kama Shule,Soko  na maeneo
ya  wazi.

No comments:

Post a Comment