Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday 8 September 2015

MTOTO ALIYEIBWA APATIKANA BAADA YA MIEZI MINNE


Mahakama nchini El Salvador imeamuru mtoto aliyebadilishwa punde baada ya kuzaliwa kukutanishwa na wazazi wake halisi miezi minne baadaye.
Mahakama hiyo iliamuru uchunguziwa kina kufanyika kuhusiana na daktari aliyeshutumiwa na mama kwa kumbadilishia mtoto wake wakati wa kujifungua.
Mama huyo, Mercedes Casanella,anasema kwamba mtoto aliyemuona muda mfupi baada ya kujifungua mwezi May alikua na ngozi nyeupe na maumbile
tofauti na yule aliyekabidhiwa baadae .
Mtoto Mweusi
''Mtoto niliyemuona alikuwa na rangi ya hudhurungi lakini yule aliyeletwa alikuwa ni mweusi titi ti''
Kipimo cha vinasaba DNA kimethibitisha kwamba mtoto huyo mchanga si wa mwanamke huyo kibayolojia.
Bi Casanella anasema kuwa daktari huyo Alejandro Guidos alikuwa amekusudia kufanya mabadiliko hayo.
Image captionRichard Cushworth na mkewe Mercedes Casanella
Vyombo vya habari nchini humo vinasema kwamba matokeo ya uchunguzi wa vinasaba umebaini mtoto huyo si wa bi Casanella na mumewe.
Aidha hayo yalitiliwa pondo na matokeo ya uchunguzi uliofanywa kwa watoto wote waliozaliwa katika zahanati hiyo ya afya katika siku hiyo moja.
Wazazi wa mtoto huyo wamemshutumu dakatari , Alejandro Guidos, kwa kumuuza mtoto wao mweupe kwa wafanyabiashara haramu ya watoto , lakini alikana kufanya kosa lolote.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment