Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday, 10 December 2014

DEREVA WA BODABODA ANYAKUA BAJAJ LIMO YA SERENGETI

Displaying 1.JPG
Meneja wa Bia chapa ya Serengeti, Rugambo Rodney katikati  akithibitisha namba ya simu ya mkononi  ya mshindi wa Limo Bajaj, wakati wa kuchezesha droo hiyo ya  “tutoke na Serengeti” (kulia) ni Mkaguzi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha,  Abdallah Hemed, na kushoto ni Mkaguzi kutoka Pricewatercoopers, Golder Kamuzora. Hafla hiyo ilifanyika makao makuu ya Serengeti jijini Dar es Salaam.

Displaying 2.JPG
Mkaguzi toka Pricewatercoopers, Golder Kamuzora akithibitisha namba ya mshindi wa Limo bajaji, wakati wa kuchezesha droo ya kumtafuta mshindi wa pili wa limo bajaj, katikati ni Meneja wa Bia chapa ya Serengeti, Rugambo Rodney na kulia ni Mkaguzi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Abdallah Hemed. Hafla hiyo ilifanyika Serengeti mjini Dar es Salaam.
Displaying 3.JPG
Meneja wa bia chapa Bia ya Serengeti, Rugambo Rodney , akiongea kwa simu na mshindi wa Limo bajaj ya Pili kutolewa katika shindano la “Tutoke na Serengeti” Peter Emanuel mkazi wa Rombo Kilimanjaro katika shindano linaloendeshwa na ka mpuni hiyo ya bia ya Serengeti. Kulia ni Mkaguzi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Abdallah Hemed. Hafla hiyo ilifanyika Serengeti mjini Dar es Salaam.
Displaying 4.JPG
Meneja wa bia chapa Bia ya Serengeti, Rugambo Rodney , akifafanua jambo wakati wa kuchezesha shindano la” Tutoke na Serengeti” ambapo Peter Emanuel mkazi wa Rombo mkoani nkilimanjaro ameibuka mshindin kwa kujinyakulia Limo Bajaj yenye thamani ya Sh. 7 milioni. Kulia ni mkaguzi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Abdullah Hemed.  
Displaying 5.JPG

Meneja wa bia chapa Bia ya Serengeti, Rugambo Rodney, katikati akifafanua jambo wakati wa kuchezesha shindano la” Tutoke na Serengeti” ambapo Peter Emanuel mkazi wa Rombo mkoani nkilimanjaro ameibuka mshindin kwa kujinyakulia Limo Bajaj yenye thamani ya Sh. 7 milioni. Kulia ni mkaguzi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Abdullah Hemed  na kushoto ni Mkaguzi toka Pricewatercoopers, Golder Kamuzora. Hafla hiyo ilifanyika makao makuu ya Serengeti, jijini Dar es Salaam.

Mkazi wa Rombo Bwana Peter Emmanuel mwenye miaka 37 ameibuka mshindi wa pili wa Limo Bajaj katika droo ya pili ya kampeni ya miezi mitatu ijulikanayo kama “Tutoke na Serengeti”, inayodhaminiwa na Serengeti Breweries Ltd ikishirikiana na B-Pesa.
“Ninafuraha sana pia namshukuru Mungu...hii ni siku nzuri sana kwangu. Asante Serengeti kwa zawadi hii na ninaahidi kuendelea kushiriki katika promosheni hii, hata ikiwezekana kushinda bajaji nyingine.” Alisema Bajaj hiyo itamuongezea kipato kwa zaidi ya asilimia 30. Mara tu baada ya kutaarifiwa kwa njia ya simu kwamba amejishindia Limo Bajaj. Sambamba na hilo Bi Valerian Moshi mkulima wa Moshi vijijini ni mshindi mwingine aliyejipatia Tsh. 100,000/=
Kampeni hii ya nchi nzima ilizinduliwa rasmi na kampuni ya SBL pamoja na B-Pesa mwanzoni mwa mwezi uliopita na imekuwa ikiwazawadia wateja wake kila wiki katika kila  droo iliyokuwa ikifanywa na SBL chini ya usimamizi wa bodi ya michezo ya bahati nasibu Tanzania.
Baadhi ya washindi waliofaidika na kupata zawadi  katika kampeni hii ni pamoja na  : -Bi. Rukia Almasi ambaye ni mama wa nyumbani na mkazi wa Kihonda aliyejishindia  Limo Bajaj ya kwanza na Hassan Mfaume aliyeshinda safari ya siku mbili kutembelea Serengeti National park ambayo itaigharimu  SBL takriban Tsh 10 milioni.
Akizungumza na vyombo vya habari, Bwana. Rugambo Rodney-Meneja chapa wa bia ya Serengeti Premium Lager alisema, “kadiri kampeni inavyoendelea, watu wengi wataendelea kushinda zawadi mbalimbali. Zaidi ya bajaji, zawadi nyingine ni pamoja na:- safari ya bure kwa wapenzi kutembelea hifadhi za taifa, fedha taslim za papo kwa papo za thamani ya shilingi 5,000/= , punguzo la shilingi 300/= katika gharama halisi ya bia pamoja na bia za bure zinazopatikana katika baa zote nchi nzima”.
Rodney aliendelea kusema kwamba, kwa miaka mingi sasa, Serengeti imekuwa ikiamini katika kurudisha kiasi cha faida kwa jamiii kupitia kampeni mbalimbali ambapo Tutoke na Serengeti imelenga katika hilo”.
Ujumbe toka kwa Meneja Masoko wa kampuni ya  B-Pesa Mwana. Salil Abbas ulisema kuwa bado zipo Limo Bajaj 5 za kushindaniwa na kuwashauri watanzania kuendelaea kushiriki katika kampeni .Kwenye promosheni hii, B-Pesa inahusika na usambazaji wa fedha kwa washindi kwa njia ya simu za mkononi.

Ili kushiriki katika kampeni, mteja anatakiwa awe na umri wa zaidi ya miaka 18. Kuingia katika droo na kushinda zawadi mbalimbali mshiriki anatakiwa anunue bia ya Serengeti Premium Lager na kutuma number atakazozikuta chini ya kizibo kwa ujumbe mfupi wa maneno kwenda number  15317. Kadiri utumavyo number zilizo katika kizibo ndivyo unavyojiweka katika nafasi ya kushinda. 

No comments:

Post a Comment