Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday 6 February 2016

SDL RAUNDI YA 7

Raundi ya saba ya Ligi Daraja la Pili nchini (SDL) inaendelea wikiendi hii kwa michezo 12 kuchezwa nchini, kwa timu 24 kusaka pointi kutoka makundi ya A,B,C na D kuwania nafasi nne za juu ili kuweza kupanda ligi daraja la kwanza msimu ujao.
Kundi A, Leo Ijumaa Abajalo Tabora watakua wenyeji wa Mvuvumwa uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Tabora, Green Warriors dhidi ya Singida United uwanja wa Mabatin Mlandizi (jumatatu) na Mirambo FC watacheza dhidi ya Transit Camp siku ya jumatatu uwanja wa Ali Hassani Mwinyi mkoani Tabora.
Kundi B, Kesho Jumamosi AFC ya Arusha watakua wenyeji wa Alliance Schools uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Madini FC watacheza dhidi ya JKT Rwamkoma uwanja wa Mbulu, huku Bulyanhulu FC watawakaribsiha Pamba FC uwanja wa Kamabrage mjini Shinyanga.
Kundi C, Leo Ijumaa Abajalo Dar watacheza dhidi ya Mshikamano uwanja wa Karume jijini Dar es salaam, kesho Jumamosi Kariakoo FC watawakaribisha Changanyikeni katika uwanja wa Ilulu – Lindi, na Cosmopolitani watacheza dhidi ya Villa Squad siku ya jumatatu katika uwanja wa Karume jijini Dar es salaam.
Kundi D, Jumamosi Mighty Elephant watacheza dhidi ya Wenda FC uwanja wa Majimaji mjini Songea, Mbeya Warriors watawakaribisha Mkamba Rangers uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, huku Jumapili Sabasaba FC wakicheza dhidi ya African Wanderers uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

No comments:

Post a Comment