Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ambaye ni Mkuu wa Wilaya
ya Songea Mh.Norman Sigala King aliyesimama akiongea na Vijana wa Halmashauri
ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma akifungua mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana
(hawapo pichani) ya kujikomboa kiuchumi yanayotolewa na Wizara ya Habari,
Vijana, Utamaduni na Michezo, wa kwanza kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa, Bi. Wenisaria Swai.
Kaimu Mkurugezi wa Halmashauri ya Songea Bi.
Wenisaria Swai wa kwanza kulia akiongea na ujumbe kutoka Wizara ya Habari,
Vijana, Utamaduni na Michezo wakati wa ziara ya ujumbe huo uliopo mkoani Ruvuma
kwa lengo la kutoa elimu ya ujasiriamali,Mfuko wa Maendeleo ya Vijana, Stadi za
Maisha na uongozi kwa Vijana wa Halmashauri zote za Mkoa wa Ruvuma, wa kwanza
kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria kutoka Wizarani Bi. Ester Riwa.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Songea Bw. Rajab Mtiula
wa nne kutoka kushoto waliokaa akiwa katika picha ya pamoja na vijana wa
Halmashauri ya Songea wakati mafunzo ya ujasiriamali na jinsi ya kujikomboa
kiuchumi yanayotolewa na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.
Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria Bi. Ester Riwa
kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo aliyesimama akitoa mada
ya ujasiriamali kwa Vijana wa Halmashauri Songea wakati Wizara ya Habari,
Vijana, Utamaduni na Michezo ilipofanya ziara ya mafunzoa ya kujikomboa
kiuchumiMkoani Ruvuma.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ambaye ni Mkuu wa
Wilaya ya Songea Mh.Norman Sigala King akisalimiana na baadhi ya vijana wa
Halmashauri ya Songea wakati wa mafunzo ya kujikomboa kiuchumi yanayotolewa na
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo. (Picha zote na Benjamin Sawe).
Vijana nchini wametakiwa kukopa na kurejesha mikopo
kwa wakati ili waweze kujikwamua kiuchumi.
Hayo yamesemwa na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mh.
Noman Sigala King wakati wa mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana wa Wilaya ya
Songea mkoani Ruvuma.
Mh. King alisema Serikali imeamua kutoa mafunzo kwa
vikundi vya vijana ya jinsi ya kuandaa maandiko ya miradi mbalimbali, uongozi
bora na stadi za maisha ili kuwatoa katika mitazamo hasi kwenda mitazamo chanya
kwa kutumia fursa zilizopo.
Amesema vijana wengi wanafursa mbalimbali za
kujikwamua na umaskini lakini hawatumii fursa hizo vizuri na kubakia wakikaa
vijiweni bila kujishughulisha na kazi yeyote na kuishia kuvuta madawa ya
kulevya na kuwa wezi.
Nea Diwani wa kata ya Matimila jimbo la Peramiho Mh.
Menesi Komba amesema mafunzo ya kujengewa uwezo ni fursa kwa vijana wa
Halmashauri ya Songea kwani watakuwa wamepewa uelewa mkubwa wa jinsi ya
kuendesha shughuli zao za ujasiriamali kwa ufanisi na utaalamu.
Aliwaasa vijana kutekeleza elimu hiyo kwa vitendo
kwa kuwafundisha vijana wenzao ambao hawakupata bahati ya kuhudhuria katika
mafunzo hayo na kuachana na tabia ya kuwa wabinafsi wa kutoa elimu ya
ujasiriamali kwa vikundi vingine.
Nae Diwani wa kata ya Peramiho na Mwenyekiti wa
Kamati za Huduma za Jamii Mh. Isack Mwimba amesema elimu ya ujasiriamali, Mfuko
wa Maendeleo ya Vijana ikiwa ni pamoja na Stadi za maisha vitawawezesha vijana
wa Halmashauri ya Songea kuwa wazalendo katika kuitumikia nchi yao na kujiinua
kiuchumi.
”Jamani vijana wenzangu ifikie muda wa kujiuliza
tutaifanyia nini nchi yetu badala ya kubakia na mawazo ya nini serikali yetu
itatupatia”. Alisema Mh. Mwimba
No comments:
Post a Comment