Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday 16 February 2016

WIZARA YA MAMBO YA NDANI YATOA TAMKO KUHUSU WAKIMBIZI NCHINI


Na Beatrice Lyimo-MAELEZO
Dar es Salaam.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imetoa tamko kuhusu hali ya wakimbizi nchini kuanzia mwezi Aprili mwaka 2015 hadi tarehe 10 Februali, 2016.
Akitoa tamko hilo leo jijini Dar es salaam Msemaji wa Wizara hiyo Isaac Nantanga  amesema kuwa  Serikali imekuwa ikipokea raia toka Burundi wanaoingia nchini Tanzania  kutokana na machafuko yaliyotokea nchini humo.

“Kiasi cha wakimbizi 129,210 toka nchini Burundi wameingia  nchini kuomba hifadhi kutokana na machafuko yaliyotokea nchini mwao  tangu mwezi  Aprili mwaka jana hadi sasa” alisema Nantanga.

Nantanga ameongeza kuwa kati ya wakimbizi 129,210, wakimbizi 79,290 wanahifadhiwa katika kambi ya wakimbizi Nyarugusu Mkoani Kigoma na wengine 45,487 wanahifadhiwa katika kambi ya wakimbizi ya Nduta iliyopo Wilayani Kibondo na 4,543 wanahifadhiwa katika kambi ya wakimbizi Mtendeli iliyopo Wilayani Kakonko. 

Ameeleza kuwa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) na wadau wengine imekuwa ikitoa huduma muhimu kama vile za afya, chakula, maji na ulinzi ili kuhakikisha wakimbizi wanaishi kwa usalama.

Mbali na hayo Tanzania inawakimbizi wengine ambao wapo katika kambi ya Nyarugusu ikijumuisha Wakongo 61,887, Wasomali 150 na wengine 189 toka katika nchi mbalimbali na kupelekea nchi ya Tanzania kuwa na jumla ya wakimbizi 191,436 ambao wamehifadhiwa katika makambi.

Wizara ya Mambo ya Ndani imeendelea kushughulikia Raia wa nchi za nje walioomba vibali cha kupatiwa hifadhi ya ukimbizi, hivyo maombi 815 yameshashughulikiwa na Kamati ya Kitaifa kuona kama wanastahili kupewa hadhi ya ukimbizi.

No comments:

Post a Comment