Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday 2 February 2016

WASANII WATAKIWA KUEPUKA RUSHWA KWENYE KAZI ZA SANAA

Msanii mshindi wa shindano la Airtel Trace Music Star Mayunga Malini (Kulia) akiongea na wadau wa Sanaa (hawako pichani) mapema wiki hii kwenye programu ya Jukwaa la Sanaa ya Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA). Wengine katika picha ni Afisa Habari wa BASATA, Aristides Kwizela (Katikati) na Afisa Sanaa wa Baraza hilo Augustino Makame.


Msanii Mayunga Malimi akiimba wimbo wake wa Nice Couple sambamba na mkongwe wa muziki wa dansi nchini Kassim Mapili kwenye programu ya Jukwaa la Sanaa la Baraza la Sanaa la Taifa mapema wiki hii.

Msanii mkongwe wa Sanaa za Maonesho Nkwama Ballanga akimpongeza Msanii Mayunga kwa juhudi zake na kujituma katika kazi anazofanya. Wadau wengi wa Sanaa waliohudhuria kwenye programu ya Jukwaa wiki hii walifurahishwa na juhudi binafsi za Msanii Mayunga.


Sehemu ya wadau wa Sanaa waliohudhuria programu ya Jukwaa la Sanaa wakimfuatilia kwa makini Msanii Mayunga.

Na Mwandishi Wetu
Wasanii nchini wametakiwa kujituma na kutengeneza kazi za Sanaa zenye ubora na kuachana na dhana ya kutegemea rushwa na hongo katika kuyafikia mafanikio yao kisanaa.
Wito huo umetolewa mapema wiki hii na wadau wa Sanaa kwenye programu ya Jukwaa la Sanaa ambayo huandaliwa na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) na kufanyika kwa mwezi mara mbili siku ya Jumatatu kwenye ukumbi wa Baraza hilo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wadau hao walisema kwamba kumekuwa na wimbi la wasanii na mameneja wa wasanii kutegemea rushwa za fedha na wengine kufikia hatua kutoa rushwa za ngono ili kufanikiwa kisanaa hasa katika kuvishawishi vituo vya radio na televisheni kucheza nyimbo zao.
“Ukweli ni kuwa rushwa na hongo zinaendekezwa na wasanii walioshindwa. Msanii anayejitambua hawezi kutoa rushwa ili wimbo wake uchezwe. Lazima wasanii waachane na dhana hii potofu, waelewe kwamba kazi ya Sanaa iliyo bora itapendwa tu na kukubalika na jamii” alisema Nkwama Bhallanga ambaye ni Msanii wa Sanaa za Maonesho.
Kwa upande wake Katibu wa chama cha wachezesha disko (TDMA) Asanterrabi Mtaki alisema kuwa dhana kwamba wasanii lazima wahonge watangazaji au ma DJs ili nyimbo zao zichezwe ni potofu na ni chanzo cha kutangaza muziki au kazi za Sanaa zisizo bora na kuziacha zile zenye ubora.
“Kama wimbo wako ni mzuri kwa nini uhonge au utoe rushwa ili uchezwe? Hapa ndipo tatizo la kuendekeza kazi mbovu za Sanaa linapoanzia. Muziki wa wenye fedha na wanaohonga ndiyo unasikika, ule mzuri unaondaliwa na wasanii wasiyo na uwezo haupati nafasi” alisema Mtaki.
Alitoa wito kwa wasanii kufikiria njia mbadala za kutangaza nyimbo zao hasa kumbi za disko badala ya kutegemea vituo vya radio pekee.
Awali akizungumza kwenye Jukwaa la Sanaa, Msanii na mshindi wa shindano la Airtel Trace Music Star Mayunga Malini alisema kuwa wasanii hawana budi kujituma, kutafuta fursa na kuzitumia ipasavyo hasa kwa kutumia muda mwingi kubuni kazi zenye ubora.

Aliongeza kuwa, wasanii hawana budi kuachana na dhana ya utegemezi na kutegemea fedha na hongo katika kupata mafanikio kwani kazi za Sanaa zikitengenezwa kwa ubora na kwa kuzingatia vigezo vyote zitapendwa na kutuzwa tu. 

No comments:

Post a Comment