Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday 12 February 2016

RWANDA KUWAHAMISHA WAKIMBIZI WA BURUNDI

Rais Paul Kagame wa Rwanda
Serikali ya Rwanda imetangaza kwamba itawahamisha mara moja wakimbizi wa Burundi hadi mataifa mengine.
Waziri wa maswala ya kigeni Luoise Mushikwabo amesema kuwa ukosefu wa maelewano haukubaliki ,baada ya mjumbe mmoja wa Marekani kuzungumzia kuhusu ripoti kwamba Rwanda imekuwa ikiwapa mafunzo wakimbizi wa Burundi ili kukabiliana na serikali ya Burundi.
Rwanda kwa sasa inawahifadhi makumi ya maelfu ya wakimbizi katika kambi.
Taarifa ya serikali imesema kuwa uwepo wao katika himaya yake,ikiwa ni karibu na taifa lao,ni hatari kwa wahusika wote.

Image copyrightReuters
Image captionWakimbizi wa Burundi

Wiki iliopita wataalam wa Umoja wa Mataifa waliliambia baraza la usalama la umoja wa mataifa kwamba Rwanda imewasajili na kuwapa mafunzo wakimbizi kutoka Burundi wakiwemo watoto ambao walitaka kumuondoa rais wa Burundi Pierre Nkurunziza kutoka madarakani.
Burundi kwa mara kadhaa imeilaumu Rwanda kwa kuwaunga mkono waasi walio na lengo la kuipindua serikali ya Bujumbura.
Hatahivyo Kigali imekana madai hayo.

Image copyrightAFP
Image captionRais Pierre Nkurunziza

''Rwanda imechukua jukumu la kuwalinda na kuwaangalia wakimbizi'',ilisema taarifa ya serikali.
Hatahivyo imebainika katika eneo la maziwa makuu kwamba uwepo wao kwa kipindi cha mda mrefu karibu na taifa lao ni hatari kwa wahusika wote.
Taifa la Burundi limekuwa katika vita vya wenyewe kwa wenyewe tangu Nkurunziza kutangaza mipango mwezi Aprili kuwania muhula wa tatu,ambao alishinda.Mamia ya raia wameuawa na wengine 230,000 kulitoroka taifa hilo.

Image copyrightReuters
Image captionMaandamano ya Burundi

Rwanda inawahifadhi zaidi ya wakimbizi 70,000 ikiwemo 24,000 wanaoitwa wakimbizi wa mijini.Kambi kubwa ya wakimbizi nchini humo ni ile ya Mahama.
Hakuna kambi nyengine zozote za wakimbizi zinazojulikana isipokuwa kambi ndogo za muda kwa wale wanaongojea kupelekwa katika kambi ya Mahama.
BBC

No comments:

Post a Comment