Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 17 February 2016

BASATA LAMPONGEZA MSANII ALIYETEMBEA KWA MIGUU KUTOKA MWANZA KUMPONGEZA RAIS JPM

Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Godfrey Mungereza (Kushoto) akizungumza na Msanii Joseph Stanford ofisini kwake mapema wiki hii. Msanii huyu ametembea kwa miguu kutoka Mwanza hadi Dar es Salaam kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli.



Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) akimkabidhi cheti cha usajili Msanii Joseph Stanford aliyetembea kwa miguu kutoka Mwanza hadi Dar es Salaam kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mitaji na Misaada kwa wasanii Bi. Elineka Ndowo. 

NEWS RELEASE

BASATA LAMPONGEZA MSANII JOSEPH STANFORD ALIYETEMBEA KWA MIGUU KUTOKA MWANZA HADI DAR ES SALAAM KUMPONGEZA RAIS MAGUFULI

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limempongeza Msanii Joseph Stanford kutoka Mwanza aliyetembea kwa miguu umbali wa zaidi ya kilometa 1200 kumpongeza Rais Dkt. John Pombe Magufuli kutokana na utendaji wake pia uundaji wa Idara ya Sanaa iliyo chini ya Wizara ya Habari, Michezo, Sanaa na Utamaduni.
Aidha, BASATA imempa zawadi ya usajili bure msanii huyu ili atambuliwe rasmi katika tasnia ya Sanaa na baadaye kufanya kazi zake kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za sekta hii.
Akizungumza ofisini kwake, Katibu Mtendaji wa BASATA Godfrey Mngereza alisema kuwa Stanford ameonesha uzalendo wa hali ya juu kwa nchi yake kwani haikuwa kazi rahisi kutembea umbali mrefu na usiku na mchana kuja kumpongeza Rais Dkt. Magufuli.
“Sisi kama Baraza tunafarijika sana, tunafurahi kuona wasanii na vijana kwa ujumla mnakuwa wazalendo na kufurahishwa na kasi ya utendaji wa Serikali ya awamu ya tano. Tunafurahi zaidi unapopeleka ujumbe wa Wasanii kwamba wamefurahia  kuundwa kwa idara ya Sanaa” alisema.
Aliongeza kuwa BASATA limetambua uzalendo na moyo wake wa kuipenda Sanaa hivyo limeamua kumpa zawadi ya usajili bure ili iwe chachu ya kujikita kwenye Sanaa na kufanya kazi zake kwa weledi na kuzingatia maadili ya kitanzania.
Kwa upande wake kijana Stanford alisema kwamba anafurahia kwa mapokezi aliyopewa na BASATA huku akisisitiza kuwa ndoto yake ni kumfikishia salamu za pongezi Mheshimiwa Rais Dkt. John Magufuli lakini pia kupata mafanikio kwenye kazi za Sanaa.
“Nafurahi sana kwa mapokezi niliyopata, muda wowote nitaenda kumfikishia salamu za pongezi Rais wangu. Matumaini yangu ni kuona sekta ya Sanaa inazidi kuthaminiwa na kusonga mbele” alisisitiza Stanford.

Msanii Stanford anatokea eneo la Mabatini jijini Mwanza na ametembea kwa siku ishirini na tano kutoka Mwanza hadi Dar es Salaam na ametumia kiasi cha shilingi elfu arobaini na tano pekee. 

No comments:

Post a Comment