Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday 24 July 2015

RAIS BARACK OBAMA AWASILI KENYA USIKU HUU, ASAINI KITABU CHA WAGENI UWANJA WA NDEGE

Rais Obama
Rais Obama akisaini kitabu cha wageni katika uwanja wa JKIA
Rais Barrack Obama wa Marekani, tayari amewasili mjini Nairobi.

Ndege iliyombeba rais obama ilitua katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta muda mfupi baada ya saa mbili za usiku.
Alipowasili Rais Obama amelakiwa na mweyeji wake Rais Uhuru Kenyatta.
mwendo wa saa mbili na robo rais Obama alitua ndege yake.
Alipowasili alizungumza kwa muda mfupi na mwenyeji wake rais Kenyatta na kisha kutia saini kitabu cha wageni kabla ya kuondoka.
Ndege ya Obama katika Uwanja wa JKIA
Obama sasa ameandikisha historia ya kuwa rais wa kwanza wa Marekani, kuzuru Kenya akiwa ofisini.
Obama anatarajiwa kufungua mkutano wa sita wa kimataifa kuhusu ujasiri mali katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini Nairobi.
Baadaye rais huyo atafanya mashauriano na rais Uhuru Kenyatta katika ikulu ya Nairobi.
Siku yan Jumapili rais Obama atahutubia mkutano wa wakuu wa mashirika ya kijamii katika chuo kikuu cha Kenyatta kabla ya kuhutubia mkutano mwingine kwa wakenya wote katika uwanja wa Kasakani.
Obama anatarajiwa kuondoka siku ya Jumapili kuelekea nchini Ethiopia.
Maelfu ya wakenya wamejipanga kando ya barabara kuu inayotoka uwanja wa ndege ili kumlaki rais huyo wa Marekani, ambaye anarejea nchini Kenya ambako babake alizaliwa.
Wakenya wakifuatilia ziara ya Obama kwenye runinga
Mamilioni ya Wakenya wengine naowalifuatilia kuwasili kwake kwenye runinga.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment