Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday 25 July 2015

OBAMA KUFUNGUA MKUTANO WA BIASHARA KENYA

Rais Obama akishuka kwenye ndege jana usiku
Rais wa Marekani Barrack Obama anatarajiwa kufungua mkutano mkubwa wa kibiashara katika siku ya kwanza ya ziara yake ya kipekee nchini Kenya.

Amepongeza kile alichokitaja kuwa maendeleo ya kibiashara na anatarajiwa kusisitiza kuhusu vita dhidi ya ufisadi nchini.
Atazuru eneo la kumbukumbu za bomu katika eneo la uliokuwa ubalozi wa Marekani kabla ya mazungumzo kuhusu usalama na rais Uhuru Kenyatta.
Rais Obama akijumuika na familia yake muda mfupi alipowasili Kenya.
Rais Obama aliwasili mjini Nairobi siku ya ijumaa kwa ziara yake ya kwanza akiwa rais nyumbani kwa babaake huko.
Ziara hiyo imetajwa kuwa ya kurudi nyumbani na vyombo vya habari na makundi ya raia walioushangilia msafara wa Obama wakati ulipokuwa ukitoka katika uwanja wa ndege wa Jomo kenyatta Jijini Nairobi.
Siku ya jumamosi ,rais huyo wa Marekani ataongoza ufunguzi wa mkutano mkubwa wa kibiashara ,baadaye rais Obama atazuru eneo la kumbukumbu katika uliokuwa ubalozi wa Marekani.
Rais Obama
Zaidi ya watu 200 waliuawa ikiwemo raia 12 wa Marekani pamoja na wafanyikazi 34 wa ubalozi huo wakati wa shambulizi hilo lililodaiwa kutekelezwa na kundi la Alqaeda.
Shambulizi jengine kama hilo lilifanyika sambamba na lile la Nairobi la jijini Dar-es-Salaam Tanzania ambapo takriban watu 11 waliuawa na wengine 70 wakijeruhiwa.
Baadaye rais Obama anatarajiwa kufanya mazungumzo ya kibiashara na mwenzake wa Kenya Uhuru Kenyatta.
Rais Obama
Mwandishi wa BBC Karen Allen anasema kuwa ni maswala ya usalama na mikakati ya kukabiliana na ugaidi ndio yatakayotawala mazungumzo hayo.
Kenya imelengwa na wapiganaji wa Alshabaab ambao wamewaua takriban watu 67 katika shambulizi lililotekelezwa katika duka la West Gate mnamo mwaka 2013.
Kundi hilo pia lilitekeleza shambulizi katika chuo kikuu cha Garissa,kazkazini mwa Kenya mapema mwaka huu ambapo liliwaua watu 148.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment