Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday 4 July 2015

BIDHAA ZAUZWA BILA NEMBO YA TBS

Baadhi ya bidhaa zinazouzwa bila nembo ya ubora ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS).
Soko la Tanzania limekuwa likipokea bidhaa kutoka ndani na nje ya nchi lakini baadhi ya bidhaa zinaarifiwa kuuzwa madukani huku zikikosa nembo za ubora.
Baadhi ya bidhaa hizo pia zimeonekana kuuzwa katika maonyesho ya kimataifa ya biashara yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
Katika maonyesho kama hayo ya biashara ya saba saba nchini Tanzania huwa ni fursa ya wafanyibiashara na wajasiriamali kuonyesha bidhaa zao mbali mbali lakini kwa wengine huwa wanatumia fursa hiyo kusambaza na kuuza bidhaa duni kwa bei ya kutupa.
katika maonyesho hayo bidhaa hizo na nyingine zinaendelea kuuzwa huku kukiwa na sheria na utaratibu kamili .
Bi Roida Andusamile ni msemaji wa shirika la viwango Tanzania na anasema hali halisi ni kwamba kuna baadhi ya wajasiriamali ambao wanaonyesha biashara zao wakati bidhaa zao hazijathibitishwa na shirika la viwango kuwa zina ubora.
Hata hivyo viongozi wa maonyesho hayo wanasisitiza kuwa wameweka uthibiti wa kutosha ili kukinzana na tatizo hili la bidhaa feki katika maonyesho hayo ya biashara.
Ingawa baadhi ya wafanya bishara wanakiri kukosa kiambishi cha kuonyesha ubora wa bidhaa zao zinawanyima soko , sio nyumbani tu lakini hata kimataifa kwa kuwa uwezo wao bado ni mdogo ingawa bidhaa zao zina ubora.
Wakati maonyesho hayo yakiendelea, maafisa wa serikali wanachukua fursa ya kuwepo kwenye maonyesho na kutoa mafunzo kuhusu ubora wa bidhaa .
Mamlaka ya chakula na dawa inasema iko makini katika hilo kwani maafisa wao bado hutembelea mabanda ili kubaini bidhaa feki zilizoingia.
Afisa wa uelimishaji jamii;James Ndege anasema sio vyema kuwalaumu wafanyabiashara pekee yao kutokana na tatizo hili kwani tatizo la bidhaa feki linamgusa kila mmoja.
Hata hivyo bidhaa hizi zisizo na viwango zimekuwa ni changamoto kwa kuwa na athari nyingi kiafya na usimamizi wake kuwa mgumu.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment