Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday, 4 October 2014

SERENGETI FIESTA SINGIDA “NI SHEEDAH”

Ney wa Mitego akishambulia jukwaa Singida
Stamina na Ney wa Mitego wakiimba pamoja 

Baraka da Prince naye hakuwa nyuma 
Mr Blue

 Wananchi wa mkoa wa Singida wamethibitisha kuwa mashabiki wa kweli katika nyanja za burudani baada ya kujitokeza kwa wingi katika tamasha la Serengeti Fiesta lilifanyika katika uwanja wa Namfua Oktoba 03, mwaka huu.
Kutokana na umati mkubwa uliojitokeza mwaka jana mjini Singida, wadhamini wakuu wa tamasha hilo, kampuni ya bia ya Serengeti kupitia kinywaji chake maarufu cha Serengeti Premium Lager waliamua kuwarudisha nyuma mashabiki wa mkoa huo kwa kuwapa shoo kali.
Kwa mara nyingine tena Singida walifanikiwa kuweka historia  katika mfululizo wa matamasha hayo miaka ya hivi karibuni kwa kujitokeza kwa idadi kubwa, tiketi zilinunuliwa tangu saa 10 alasiri toka kwa wauzaji na mashabiki waliokuwa na shauku kubwa ya kushuhudia burudani.
Wasanii waliojitokeza kuisindikiza SBL katika shoo hiyo ni pamoja na “Mwana Fa, Nikki II, Makomando, Stamina, Ney, Young Killa, Linah, Recho, Mr. Blue, Dully Sykes, Mo Music, Baraka Da Prince, Supa Nyotas:- (G-Luck, K-Style and Edo boy) ambao walitoa burudani safi iliyoacha gumzo kwa mashabiki wa Singida na vitongoji vyake.
Makomando, Ney na Stamina ni baadhi ya wasanii waliowashika mashabiki wa mkoa huo kwa shoo kali wakati walipopanda katika jukwaa na kutumbuiza na nyimbo kama “Kibababa” na “Huko kwenu vipi” ambazo ziliwakamata vilivyo mashabiki wa burudani uwanjani hapo. Dully Sykes ni msanii mwingine aliyewakamata mashabiki kwa kutoa burudani nzuri mara baada ya kupanda jukwaani na kuwafanya waimbe pamoja nae na kumshangilia alipokuwa akiimba.
“Tamasha la Serengeti Fiesta hapa Singida limegeuka kuwa la kushangaza kwetu kama waandaaji na kiukweli hii ni moja ya shoo kali na ya kusisimua ambayo hatukutarajia kama ingewafurahisha mashabiki wetu wa Singida kiasi hiki,”....alithibitisha Ndugu Rugambo Rodney, Meneja Chapa Serengeti Premium Lager.
Serengeti Fiesta inatarajia kuhitimisha ziara zake za mwaka huu hapo tarehe Oktoba 18 jijini Dar es Salaam, mikoa mingine inayotarajia kupata shoo murua za Serengeti Fiesta ni pamoja Dodoma na Mtwara kama walivyo ahidi waandaji.




No comments:

Post a Comment