Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday 20 October 2014

HII SASA KALI: MAJI YA MAITI KIVUTIO CHA BIASHARA


Mortuary

Katika tukio la kushangaza na la kutaka kujiongezea mapato pamoja na kushamiri kwa biashara,wafanyibiashara wawili katika mtaa wa Lobengula nchini Zimbabwe walizozania maji machafu yanayopatikana baada ya kuosha wafu ambayo huyatumia kuvutia wateja.
Wawili hao waliojulikana kama ViolaTshuma na Molene Hadebe walikabiliana vilivyo baada ya Hadebe kuchukua kiwango kikubwa cha maji hayo ya kuosha maiti kabla ya mwenzake kuwasili.
Wafanyibiashara hao wanaodaiwa kuwa rafiki wakubwa walipata maji hayo kutoka chumba kimoja cha mazishi katika mji wa Bulawayo kwa biashara yao ya kila siku.
Kulingana na wafanyibiashara wengine maji hayo huuzwa kwa wafanyibishara na wanawake wanaotumia kufanya tambiko.
Maji hayo pia hutumika kuwazima wanaume walio wakali kwa wake zao baada ya kubaini kwamba wake hao wanawanyemelea wanaume wengine.
Wafanyibiashara waliohijiwa pia walibaini kuwa maji hayo pia hutumiwa kuosha matunda na hata nyanya ili kuwavutia wateja wengi kama wale wanaouhudhuria mazishi.
CREDIT: BBC/SWAHILI

No comments:

Post a Comment