Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday 19 October 2014

CUBA YATUMA MADAKTARI ZAIDI KUTIBU EBOLA AFRIKA

Madaktari wa mwanzo wa Cuba walipowasili Freetown
Rais wa zamani wa Cuba, Fidel Castro, anasema nchi yake itatuma karibu madaktari na wauguzi 300 zaidi kusaidia kupambana na Ebola Afrika.

Alisema Cuba iko tayari kushirikiana na Marekani kwa masilahi ya amani duniani.
Cuba imeshatuma madaktari na wauguzi 165 huko Afrika Magharibi.
Katika tukio jengine, Shirika la Afya Duniani, WHO, limesema kuwa ripoti yake ya siri iliyofichuliwa nje ya shirika, ambayo ilidai kuwa shirika hilo lilifanya makosa katika kushughulikia janga hilo la Ebola, haikuwa kamilifu na ilikuwa bado haikuchambuliwa.
WHO imesema uchambuzi kamili wa hatua ilizochukua utakamilika baada ya ugonjwa wa Ebola kudhibitiwa.
CREDIT: BBC/SWAHILI

No comments:

Post a Comment