Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday 5 April 2016

CHACHA AJIUZULU TFF

Martin Chacha (kushoto) wakati alipokuwa mwanasheria wa klabu ya Yanga. 

Kaimu Mkurugenzi wa Mashindano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Martin Chacha amejiuzulu nafasi yake katika utumishi wa TFF kuanzia leo tarehe 5 Aprili 2016.
 
Katika barua yake aliyomwandikia Katibu Mkuu wa TFF, Chacha alieleza kuwa amepata majukumu mapya ya kikazi ambayo pamoja na majukumu ya kifamilia
yatamfanya akose muda wa kutumika vema katika nafasi yake katika Shirikisho

Martin alijiunga na TFF Julai 2014 akiwa Afisa wa Mashindano na baadaye kuteuliwa kukaimu nafasi ya Mkurugenzi wa Mashindano, kufuatia aliyekuwa anashikiria nafasi hiyo Boniface Wambura kuteuliwa kuwa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB).

TFF inamtakia kila la kheri na mafanikio mema Chacha katika majukumu yake mapya.

No comments:

Post a Comment