Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday 6 September 2014

TUME YA UCHUNGUZI WA OPERESHENI TOKOMEZA YAANZA KUPOKEA MALALAMIKO


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TAARIFA KWA UMMA

TUME YA UCHUNGUZI WA OPERESHENI TOKOMEZA UJANGILI YAANZA RASMI KUPOKEA TAARIFA NA MALALAMIKO KUHUSU UTEKELEZAJI WA OPERESHENI TOKOMEZA NCHINI
-------------------------------------
Tume ya Rais ya Uchunguzi wa Operesheni Tokomeza ujangili inatoa taarifa kwa umma kuwa imeanza rasmi kupokea taarifa na malalamiko mbalimbali kuhusu utekelezaji wa Operesheni Tokomeza Ujangili nchini.
Katika kufanikisha majukumu yake, Tume itatembelea maeneo mbalimbali nchini ili kukutana na wananchi wenye tarifa au malalamiko kuhusu utekelezaji wa Operesheni Tokomeza.

Aidha, Tume inawaarifu wananchi kuwa taarifa au malalamiko yaliyotokana na utekelezaji wa Operesheni hiyo yatapokelewa kwa njia ya posta, barua pepe na simu za mkononi kama ifuatavyo;
i. Katibu wa Tume,
Tume ya Uchunguzi wa Operesheni Tokomeza Ujangili,
SLP 9050,
Kivukoni Front,
Dar es Salaam
iii. Namba za simu
Tigo: 0714 826826
Vodacom: 0767 826826
Airtel: 0787 826826
Zantel: 0773 826826
Imetolewa na:

(signed)
Fredrick K. Manyanda
KATIBU WA TUME
5 Septemba, 2014

No comments:

Post a Comment