Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday 28 September 2014

ACHANA NA IS, KUNDI LA AL-NUSRA FRONT NALO LATANGAZA VITA!

Wapiganaji wa Jihad kutoka kundi la Al Nusra front
Kundi lililo na uhusiano na mtandao wa Al-Qaeda nchini Syria Al- Nusra Front limepinga mashambulizi ya angani yanayotekelezwa na muungano unaoongozwa na Marekani kama vita dhidi ya Uislamu na kusema kuwa nchi za Magharibi na zile za Kiarabu zinazohusika zitalengwa na makundi ya Jihad kote duniani.

Matamshi hayo yanatolewa baada ya Marekani kusema kuwa ushirikiano na washirika wake wa Kiarabu umefanya mashambulizi zaidi dhidi ya wanamgambo wa Islamic State nchini Syria na Iraq.
Wizara ya ulinzi nchini Marekani ilisema kuwa ndege za kijeshi zilishambulia mji wa Raqqa nchini Syria ambao ni ngome ya wanamgambo pamoja na maeneo yanayodhibitiwa na kundi la Islamic state karibu na mji wa Kikurdi wa Kobane karibu na mpaka na Uturuki.
CREDIT: BBC/SWAHILI

No comments:

Post a Comment