Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday 27 September 2014

CHUO CHA DINI CHAFUNGWA KENYA, CHATUHUMIWA KUFUNDISHA 'UGAIDI'!

Madrasa ya Ngulini iliyofungwa kwa madai kuwa inafunza itikadi kali za kidini
Maofisa nchini Kenya wameifunga Madrassa au shule ya mafunzo ya dini ya Kiislamu nchini humo kwa madai kuwa inafunza masomo ya itikadi kali.
Madrassa hiyo iliyo mjini Machakos, Mashariki mwa Nairobi, imechukuliwa hatua hiyo baada ya vijana kadhaa waliokuwa wakihojiwa na polisi kuitaja.

Vijana hao wanazuiliwa kwa tuhuma za kuhusiana na wapiganaji wa Kiisilamu nchini Somalia.
Kundi la Al-Shabab limekuwa likifanya mashambulio kadhaa nchini Kenya kama hatua ya kulipiza kisasi kuwepo wanajeshi wa nchini hiyo Somalia.
CREDIT: BBC/SWAHILI

No comments:

Post a Comment