Mwanamitondo afanyae kazi zake za mitindo nchini Marekani Flaviana Matata, yuko nchini kwa ajili ya kufanya kazi za kijamii kupitia taasisi yake ya Flaviana Matata Foundation. katika mradi wa Back to school project /FMFstationary kit ambao unafadhiliwa na mfuko wa penseni PSPF,
Baada ya mwezi January Flaviana kugawa vifaa shule za msingi za jijini awamu hii ameenda Mtwara na kufanikiwa kugawa shule za Msingi Mtua na Chemchem ziliyopo Nachingwea pamoja nashule za msingi Litingi na Mnengulo ziliyopo Lindi.
bado wanaendelea kugawa vifaa hivyo kwa shule za msingi mikoa mingine “hadi sasa tumeshagawa vifaa kwa watoto 700 na bado kuna kits 800 vitasambazwa Tunduma ,Tunduru na Monduli”
Flaviana alitoa shukran kwa PSPF kwa kudhamini huu mradi na akasisitiza makampuni na mashirika kujaribu kuwezesha elimu kama hali halisi inavyoonekana kwenye picha hadi leo kuna wanafunzi wanasoma chini na mti, na walio madarasani,madarasa ni mabovu na hayana madawati.
Flaviana Matata ameongozana na Meneja wa Mawasiliano, Masoko na Uenezi wa PSPF, Costantina Martin pamoja na wafanyakazi wa PSPF katika zoezi la kukabidhi vifaa hivyo. Martin
Wanafunzi wakitoka Darasani
Mwanamitindo Flaviana Matata akiwa amekaa na wanafunzi darasani
Mwanamitindo Flaviana Matata pamoja na wafanyakazi wa mfuko wa pensheni wa PSPF wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi.
Meneja wa Mawasiliano, Masoko na Uenezi wa PSPF, Costantina Martin akimkabidhi begi mmoja wa wanafunzi ambaye ni mlemavu wakati wafanyakazi wa PSPF wakishirikiana na Mwanamitindo Flaviana Matata walipokabidhi vifaa mbalimbi kwa wanafunzi wa shule za Msingi Mtua na Chemchem ziliyopo Nachingwea pamoja nashule za msingi Litingi na Mnengulo ziliyopo Lindi.
Picha ya pamoja ikapigwa
Wanafunzi wakifurahia kupata vifaa hivyo.
Wanafunzi wakiwa darasani wakijisomea chini ya mti.
Mwanamitindo Flaviana Matata akisaini kitabu cha wageni.
CREDIT SOURCE: FULLSHANGWE
No comments:
Post a Comment