Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday 30 August 2014

WAZIRI MKUU WA LESOTHO AKIMBIA MAPINDUZI, AJIFICHA AFRIKA KUSINI

Jeshi la Lesotho

Waziri mkuu nchini Lesotho Tom Thabane ameiambia BBC kwamba amelitoroka taifa hilo baada ya kupata vitisho vya maisha yake.
Akizungumza kutoka nchini Afrika kusini,Bwana Thabane amesema kuwa vitenmdo vya jeshi nchini humo vimesitisha huduma za serikali na kusababisha mapinduzi.
Uchaguzi uliozongwa na utata nchini humo miaka miwili iliopita ulisababisha kuundwa kwa serikali ya muungano isio dhabiti.Awali Ripoti kutoka mji mkuu wa maseru zilizsema kuwa jeshi lilizingira makao makuu ya polisi na kuzuia matangazo ya radio pamoja na mtandao wa simu katika mji mkuu wa Maseru.
Licha ya mazungumzo ya kuleta amani mnamo mwezi Juni ,hali ya wasiwasi ilitanda huku majirani wa taifa hiilo wakionya dhidi ya mbinu yoyote isio ya kikatiba.

Taifa hilo limezungukwa na Afrika kusini na hutegemea sana jirani yake kwa masli asli pamoja na nafasi za kazi.
BBC/SWAHILI

No comments:

Post a Comment