Leodegar Tenga
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF Jamal Malinzi,
amempongeza Bw Leodgar Tenga kwa kuchaguliwa kuendelea kuwa mjumbe wa Kamati ya
Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika (CAF).
Aidha Rais Malinzi ametuma salamu za pongezi kwa wajumbe waliochaguliwa kuwa wajumbe wapya wa
Shirikisho la Mpira wa Miguu baranai Afrika (CAF) na Shirikisho la Mpira wa
Miguu Duniani FIFA.
Katika salamu hizo na nakala zake kutumwa kwa Rais wa CAF Bw. Issa
Haytou na Rais wa FIFA Bw. Blatter, Malinzi amewatakia kila la kheri katika
majukumu hayo mapya,na kwa ajili ya
maendeleo ya mpira wa miguu duniani.
Tenga amechaguliwa nafasi hiyo baada ya kuwa mgombea pekee kutoka
kanda ya Afrika Mashariki aliyejitokeza kuwania nafasi hiyo na kuungwa mkono na
nchi zote wanachama wa CECAFA.
NB: Kesho alhamisi saa 5 kamili asubuhi kutakua na
mkutano na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Mikutano wa TFF uliopo Karume,
makocha wa Twiga Stars na She-Polopolo wataongelea maandalizi ya mwisho
kuelekea mchezo wa siku ya ijumaa.
No comments:
Post a Comment