Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday, 13 April 2015

SINAI YASHAMBULIWA KWA MABOMU MISRI

Shambulio la bomu katika rasi ya Sinai
Watu wapatao kumi na watatu wameuawa katika katika mashambulio mawili yaliyotokea kwa pamoja katika rasi ya Sinai nchini Misri.

Watu saba waliuawa na arobaini na wanne kujeruhiwa wakati bomu lililokuwa limetegwa katika gari kufyatuka katika kituo cha polisi katika mji wa al-Arish.
Mapema, saa chache bomu lililokuwa limetegwa pembeni mwa barabara liliwaua askari sita katika mji wa Sheikh Zuweid.
Kundi linalojiita "Province of Sinai" yaani Jimbo la Sinai --ambalo linachukuliwa kama tawi la Islamic State -- limesema ndilo lililofanya mashambulio yote mawili.
Wapiganaji wa kundi hili wamesema wanalipiza kisasi dhidi ya serikali ya Misri ambayo inawasaka wafuasi wa rais wa zamani wa Misri aliyeondolewa madarakani, Muhammad Morsi.
CREDIT: BBCSWAHILI

No comments:

Post a Comment