Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ndugu Paul Makonda akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar Es Salaam.
UCHUNGUZI JUU YA UBOVU WA BARABARA ZA WILAYA YA KINONDONI 13.04.2015
UTANGULIZI
Ndugu waandishi wa habari na ndugu wananchi, nimewaiteni leo, kuwaambia juu ya Agenda moja tu. Nayo ni Ubovu wa barabara.
Tangu
sijaingia ofisini hapa, na baada ya kuingia ofisi hizi za umma, kila
siku Napata fursa ya kuzunguka maeneo mbalimbali katika maeneo ya
Kinondoni, nimekuwa nikisiliza jamii nzima ya Kinondoni, wengi kero yao
kubwa ni ubovu wa barabara nchini lakini hasa wakiinyooshea kidole
wilaya yangu ya Kinondoni. Mimi nitazungumzia ubovu huo katika wilaya
yetu hii ya Kinondoni.

No comments:
Post a Comment